Serikali imesema itatumia gharama yoyote kwa ajili ya kuhifadhi Ikolojia ya bonde la mto Mara




Serikali imesema itatumia  gharama yoyote  kwa ajili  ya  kuhifadhi Ikolojia ya  bonde  la mto Mara  huku  ikisema  itatii  itifaki  ya  pamoja ya  makubaliano kati  ya  Kenya  na Tanzania katika kulinda  bonde  la mto  Mara kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo. Kutoka mugumu serengeti mkoani mara,mwanahabari wetu george marato,anayotaarifa zaidi.....Kauli hiyo imetangazwa mjini mugumu wilayani serengeti,na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa tanzania mh mizengo Peter Pinda,katika kilele za maadhimisho ya  siku ya mara ambayo  yamefanyika  kwa  mara ya  kwanza  nchini  kwa  kuhusisha nchi  za Tanzania na  kenya lengo likiwa ni kuweka mikakati  ya pamoja ya kuhifadhi  bonde  la  mto mara kwa  sababu  hiyo waziri mkuu mh mizengo  pinda,amesema  lazima serikali  za nchi  hizi  mbili wakiwemo  wadau  mbalimbali kushiriki kikamilifu katika  utunzaji  wa  bonde  la mto mara kutokana na manufaa yake  makubwa  kwa  wanyama  aina ya nyumbu  na  hivyo  kuwa kivutio kikubwa  katika  sekta  ya utalii  kwa hifadhi  za Masai Mara nchini Kenya na hifadhi  ya Taifa ya Serengeti  hapa nchini  ambayo ni moja  ya  maajabu  saba  ya  Dunia. Akitoa  salama  za  kutoka nchini Kenya, katibu mkuu wa wizara ya mazingira  na maji ya  nchi  hiyo bw James Teko, wakiwemo  wadau wanasaidia uhifadhi  wa  bonde  la  mto Mara, wamesema kuwa  juhudi  za  makusudi  zinahitajika  kwa  kila  mdau  katika  kulinda  na kuhidhi  bonde  la  mto Mara. Kauli mbiu  ya  maadhimisho  hayo  ni  Mara  ni mali  yetu  na urithi  wetu tuitunze

Post a Comment

Previous Post Next Post