Washindi 120 wapatikana kwenye droo ya kwanza ya ‘Ki-college Plus na NMB’

nmb
Meneja Huduma kwa Wateja tawi la NMB House, Joseph Massana akibofya kitufe kwenye kompyuta kuwapata washindi wa promosheni ya Ki-COLLEGE Plus na NMB wakati wa droo ya kwanza iliyo chezeshwa jana katika Makao Makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Maneja Masoko wa NMB Yusuf Shenyagwa, Afisa bidhaa wa Selcom, Everline Simpilu na Mkaguzi wa Michezo ya Kubahatisha ya Taifa, Abdallah Hemedy
Benki ya NMB jana iliendesha droo yake ya kwanza katika promosheni ya Ki-COLLEGE Plus na NMB iliyochezeshwa katika Makao Makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam. Jumla yawashindi 20 wamepata bahati ya kujishindia simu za mkononi aina ya ‘Samsung Galaxy Pocket Plus 3g’ na washindi wengine 100 kujishindia fulana za NMB.

Katika promosheni hii inayoendelea hadi tarehe 15 Januari, 2014, , wanafunzi watakaoendelea kufungua NMB Student Account wataendelea kufurahia huduma za NMB Student Account kama: Kufungua akaunti kwa Sh. 10,000 tu itakayokuwezesha kupata kadi ya ATM ya NMB), kujiunga na huduma ya NMB mobile bure, kupata huduma ya ujumbe mfupi kila utoapo fedha kwenye ATM ya NMB bure, kuchukua fedha hadi Sh.1, 000,000 kwenye NMB ATM kwa siku na kupata huduma kupitia matawi zaidi ya 150 na NMB ATM zaidi ya 500 nchi nzima.
Ili uweze kuingia kwenye droo na kupata nafasi ya kujishia Zawadi kwenye promosheni ya Ki-COLLEGE Plus na NMB, mwanafunzi wa elimu ya juu anatakiwa kufungua NMB Student Account, kuweka amana katika akaunti ya NMB Student Account, kutumia au kujiunga na NMB mobile. Ikiwa hujatumia akaunti yako kwa muda mrefu, tembelea tawi la NMB lililo karibu nawe ili uweze kupata huduma itakayokuwezesha kuanza kutumia akaunti yako, ili nawe ushiriki katika promosheni hii ya Ki-COLLEGE plus

Post a Comment

Previous Post Next Post