UTEUZI WA UONGOZI
RASIMU hii ambayo ni ndefu kuliko ya awali, madaraka ya Rais hasa ya
uteuzi yamepunguzwa kwa kuweka vyombo vya kupendekeza majina ya watu wa
kuteuliwa na kwa baadhi ya vyeo, kuhitaji kuthibitishwa na Bunge.
Rasimu hiyo yenye ibara 271 ikilinganishwa na ya awali yenye ibara
240 hata hivyo, imesisistiza Rais ndiye mwenye hadhi na heshima ya Mkuu
wa Nchi, Amiri Jeshi Mkuu na Kiongozi wa Serikali.
Vile vile imependekeza wabunge wasiwe mawaziri, kuwe na ukomo wa
uwakilishi katika Bunge na wapiga kura wawe na madaraka ya kumwajibisha
mbunge hata kabla ya kumalizika kwa muhula wake.
Mengine: Ni Spika na Naibu Spika, wasitokane na wabunge au kiongozi
wa juu wa chama cha siasa. Uraia wa Jamhuri za Muungano. Rasimu
imependekeza kutambuliwa kwa uraia wa kuzaliwa na kujiandikisha ambao ni
wa nchi mmoja.
Imependekeza kuwapo hadhi maalumu kwa watu wenye asili au nasaba ya
Tanzania ambao wameacha kuwa raia wa Tanzania kwa kuchukua uraia wa nchi
nyingine.
Marufuku kiongozi wa umma kutumia wadhifa, nafasi au madaraka kwa
manufaa yake binafsi, familia yake, ndugu, jamaa, marafiki au mtu aliye
na uhusiano naye wa karibu.
Tume kwa kuzingatia maoni ya wananchi, tofauti na ilivyokuwa katika
Rasimu ya Awali, sasa inapendekeza msajili wa Vyama vya Siasa, iwe ni
taasisi inayojitegema na isiwe sehemu ya Tume Huru ya Uchaguzi.
Imependekezwa pia, kuwepo Jeshi la Polisi moja na Idara ya Usalama wa Taifa mmoja katika Jamhuri za Muungano za Tanzania.
KIPINDI CHA MPITO
Rasimu inapendekeza muda wa mpito wa miaka minne, kuanzia tarehe ya
kuanza kutumika kwa Katiba mpya hadi Desemba 31, 2018 na kwamba sheria
zilizopo sasa zitaendelea kutumika hadi zitakapobadilishwa.
Masuala yaliyopendekezwa yafanyiwe kazi katika kipindi cha mpito
ambayo ni pamoja na kutungwa kwa Katiba ya Tanganyika na mgawanyo wa
rasilimali baina ya serikali ya Muungano na serikali za nchi washirika.
Mengine ni kufanya maandalizi ya kuendesha uchaguzi mkuu wa mwaka
2015 kwa kuzingatia masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka
2014. Kuundwa kwa Tume na Taasisi za Kikatiba, zilizoainishwa kwenye
Katiba.
Rasimu ya wananchi, akielezea mchakato wa maandalizi wa Rasimu hiyo,
Jaji Warioba alisema tofauti na wasiwasi uliyokuwapo kwa ushiriki wa
wananchi wa kawaida, ungekuwa dhaifu. Sura tano za mwanzo za Rasimu
zinatokana na mchango mkubwa kutoka kwa wananchi:
“Tume ilipoanza kulikuwa na wasiwasi kwamba ushiriki wa wananchi wa
kawaida ungekuwa dhaifu kwa sababu iliaminika kwamba wananchi kwa ujumla
wao hawana ujuzi wa Katiba,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:
“Lakini Tume iligundua mapema kwamba wananchi wanajua mambo mengi
ambayo ni msingi wa Katiba yoyote. Sura tano za mwanzo wa Rasimu ya
Katiba zinatokana na mchango mkubwa kutoka kwa wananchi,”.
Kwa mujibu wa Jaji Warioba, maoni ya wananchi yalihusu misingi ya
Taifa, tunu za Taifa, maadili na miiko ya viongozi, dira ya Taifa na
haki za binadamu.
Wananchi pia walitoa maoni mazito kuhusu uongozi na utawala wa nchi, ikijumuisha pamoja na nafasi za Wawakilishi wao Bungeni.
Ilikotoka Tume: Rais Kikwete, aliteua Tume ya Mabadiliko ya Katiba
Mpya, Aprili 6, mwaka jana 2012 ikiwa na wajumbe 34 kutoka pande zote
mbili za Tanzania, chini ya uenyekiti wa Jaji Warioba. Iliapishwa Aprili
13, 2012 na kuanza kazi rasmi Mei 2, mwaka huo huo.
Sheria ya mabadiliko ya Katiba, ilitoa miezi 18 kwa Tume, kukamilisha
kazi yake. Sheria pia ilitoa nafasi kwa Tume kuongezwa muda usiozidi
miezi miwili na iliomba muda huo ikakubaliwa kabla ya kukamilisha kazi
yake jana, na kuikabidhi kwa Rais.
Chanzo: HabariLeo
Post a Comment