KAMA SI SOKA BASI NINGEISHIA KUCHEZA SAMBA BRAZIL - WILLIAM WA CHELSEA


Close call: Spurs nearly signed Brazilian Willian before Chelsea snatched him from their grasp
“KAMA nisingekuwa staa Chelsea, ningalicheza mirindimo ya samba Brazil.” Hiyo ni kauli ya Willian Borges da Silva maarufu kama Willian, nyota wa soka wa Brazil anayekipiga Chelsea.
Brazilian boy: Willian enjoys playing the the pandeiro which, one of the most popular instruments in Brazil
Willian anasema soka ilikuwa kwenye damu kiasi cha kutotilia umuhimu wa shule, kwamba hata kazi alizopewa shuleni kwa ajili ya kuzifanya nyumbani akimpa mama yake amfanyie.

Anasema alikuwa ‘bize’ zaidi katika kucheza soka kama ambavyo wanavyofanya watoto wengi nchini Brazil, kwamba kila wakati alikuwa na mpira mguuni.
Willian anasema kuwa alitazama fainali za Kombe la Dunia 1998 akiwa na umri wa miaka tisa, na alitaka kuwa Ronaldo de Lima au Zidane ambaye alimvutia mno kwenye fainali hizo zilizofanyika Ufaransa.
“Kama nisingalifanikiwa kama mwanasoka, sina hakika ni nini ningefanya. Labda ningalikuwa napiga muziki Brazil,” alisema staa huyo anayependa kupiga ala mbalimbali za muziki kama Percussion, drum na pandeiro.
Willian mwenye umri wa miaka 25, mwenye uwezo wa kushambulia kutokea kulia, sambamba na kusaidia ulinzi na kutengeneza nafasi, amefanikiwa kuteka akili ya Jose Mourinho kiasi cha kumwamini dimbani na kumwacha benchi Juan Mata

Post a Comment

Previous Post Next Post