Msanii wa muziki kutoka Marekani, Madonna anatarajia kuhusika
katika kazi ya kuongoza filamu itakayofanyika nchini, Ade: A Love Story.
Director Madonna
Filamu hiyo ya mapenzi ni juu ya binti wa kimarekani wa miaka 19
ambaye alifika katika pwani ya Kenya na kuangukia katika penzi la kijana
wa Kiswahili aitwaye anayeitwa Ade ambaye naye anampa jina ‘Farida’ na
kuanzisha mahusiano ambayo yanakumbana na vikwazo mbalimbali. Kisa chake
kinatokana na kitabu cha hadithi cha mwandishi Rebecca Walker. Filamu
hii inaongeza rekodi ya filamu ambazo Madonna amekwishashiriki kuongoza,
ikiwemo ile ya W.E. na Wallis Simpson and Filth and Wisdom.
Post a Comment