Jee Wazanzibar muko Tayari kuivunja Serekali ya umoja wa Kitaifa GNU kwa sindikizo la ccm ?

IMG_2604
Tetesi zilizopo nikua tayari Mchawi (ccm znz) wanadaiwa mtoto wakutoa.
Hivi sasa vikao vya ccm haviishi kila kukicha , na swala kubwa ni kushambuliwa Serekali ya Umoja wa kitaifa GNU ivunjwe au kuzofiswa kwa kupangua vifungu muhimu ili baada ya hapo ife kabisa.
Hizi ni mbinu sasa wanazipanga Bara kila kukicha kwenye vikao vyao visivyo kwisha ili kutoa sindikizo kwa ccm Zanzibar waiuwe Serekali ya umoja wa kitaifa kwa kuvitengua vifungu hususani kile kilichoipa nguvu Serekali ya GNU cha 10.
Lakini ngoma imekua ngumu vipi? Ni pale Serekali ya ummoja wa kitaifa kuchaguliwa kihalali na wananchi wa Zanzibar kwa 68% , Sasa kuibadilicha kwa kutumia ubabe wao tu ccm au kuiua ni lazima urudi kwa wananchi wa Zanzibar waipigie kura tena ya maoni .
Sasa jee Wananchi wa Zanzibar muko tayari kufanya hivyo au kufanyiwa na ccm hivyo ili wapate kuwaridhisha upande wa pili wa Muungano? ,
Kwa upande wa Bara inaonekana sindikizo lakuuliwa Serekali ya umaja wakitaifa hata wasiokua ccm hivi sasa wanatiwa kampeni walikubali kwa kisingizio cha kuambiwa kua Zanzibar imevunja katiba ya Muungano kwa kujitangazia kuwa ni nchi na ina mipaka yake na Raisi wa Zanzibar kugawa mikoa.
Kwa hili Wabara wote wameshirikiana na kuwa wamoja na pindipo ccm Zanzibar kwakutumia wingi wake kwenye Baraza la Wawakilishi na kutumia ujanja wake na nguvu zake likipita basi Serekali yote ya Zanzibar imekwenda na maji (arijojo).
Maana hakutokua na nchi ya Zanzibar wala Serekali ya Umoja wa kitaifa ,tutabakiwa na jina tu la Zanzibar na litadumu kwa kipindi kifupi.
Sasa vipi tumejipanga wananchi wa Zanzibar kukabiliana na zaruba hii?
Maana tusiwategemee viongozi wa ccm Zanzibar , tayari wameshaingiwa na baridi na kauli zao hivi sasa si zamuamana na kuwategemea kuanza sasa munawajua nduguzetu hawa wanavyokua Vinyonga.
Musisahau kuwa Mtaji wa maskini ni nchi yake, Kwa hio kama hali yenyewe ni hii huu Muungano Kama ni Biashara sasa ni Hasara kwa Wazanzibar Hakuna faida kwa wananchi, Nibora tuishi kwa ujirani mwema.
Lengo la wenzetu wa Upande wa pili hivi sasa nikutusukuma tuwe nchi moja na tukikubali hivyo inamaana ndio kumezwa kwa Zanzibar na utaifa wake.
Mumesikia vitisho vya viongozi wetu wa ccm kua Muungano ukivunjika Mutakosa rasilimali zenu Bara , hii ni kuwa brainwash ili tusukumwe huko wanakotaka ,kwenye mfumo wa Serekali moja na Sote tuwe Watanganyika (Tanzania) kwa kisingizio Tanganyika imekufa kama vile tumeiua sisi Wazanzibar.
Kama Wananchi wa Zanzibar hatuko macho na ujambazi huu basi tunaweza kuipoteza Zanzibar yetu na hilo si gumu kwa ccm smz kwa vile akili zao ni zakuangalia matumbo yao tu sio hatma ya Zanzibar na kizazi cha badae.
M/mungu ibariki nchi yetu na watu wake
 

Post a Comment

Previous Post Next Post