Wakati bado juhudi zinaendelea bila mafanikio za kuitafuta ndege
ya Malaysia Airlines aina ya Boeing 777-200 iliyopotea March 8 mwaka
huu ikiwa na abiria 239, ndege nyingine ya shirika hilo imelazimika
kutua Hong Kong, china kwa dharula baada ya hitilafu za umeme kujitokeza
ikiwa safarini.
Maafisa wa shirika hilo wameiambia CNN mapema leo kuwa ndege hiyo
aina ya Airbus A330-300 iliyokuwa ikitokea Kuala Lumpur kuelekea
Incheon, Korea Kusini ililazimika kubadili njia na kwenda kutua kwa
dharula Hong Kong baada ya wafanyakazi wa ndege hiyo kugundua hitilafu
katika genereta inayozalisha umeme wa kawaida wa ndege hiyo.
Kuala Lumpur ndio uwanja wa ndege ilipotokea ndege ya shirika hilo iliyopotea ambayo hadi sasa bado haijaonekanekana.
Hata hivyo maafisa hao wameongeza kuwa pamoja na hitilafu
iliyojitokeza lakini umeme uliendelea kuzalishwa kupitia power unit
ndogo ya ndege hiyo.
SOURCE: MAIL ONLINE
Post a Comment