OFFICIAL;- BAYERN MUNICH WANYAKUWA BINGWA TENA BUNDESLIGA, GUARDIOLA ALIONJA KOMBE


Bayern Munich imetoa tena ubingwa wa Bundesliga baada ya kuicgapa Hertha Berlin kwa mabao 3-1.

Licha ya kuwa ugenini, Bayern imetwaa ubingwa huo huku ikionyesha kiwango cha juu kama ambavyo ilitarajiwa na wengi.
Kocha Pep Guardiola ambaye ni kocha wa zamani wa Barcelona, naye ameweka rekodi ya kutwaa ubingwa wa Bundesliga kwa mara ya kwanza na msimu wa kwanza akiwa kocha wa timu.

Mabao ya Bayern katika mechi hiyo yalifungwa na Toni Kroos katika dakika ya 6, Mario Goetze dakika ya 14 na Frank Ribery akamalizia kazi katika dakika ya 79 wakati lile la kufutia machozi lilifungwa na Adrian Ramos kwa penalty katika dakika ya 66.

Bayern imetwaa ubingwa huo huku ikiwa na mechi saba mkononi, hali inayoonyesha kuwa ukali wake msimu huu ilimaliza kabisa ushindani wa Ujerumani.

Post a Comment

Previous Post Next Post