Video iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa sana na mashabiki wa msanii
QUEEN DARLEEN ambaye pia ni dada wa Diamond Platnumz sasa itazinduliwa
siku ya jumapili hii tarehe 06 April, 2014 Club Bilicanas.
Video hiyo iiyoandaliwa kwa kiwango kikubwa, inategemewa
kuleta mapinduzi makubwa sana katika tasnia ya video za muziki wa Bongo
Flava hasa kwa ubunifu wake na kiwango kikubwa cha picha yenyewe kwa
muonekano.
Kwenye video hiyo wamo wasanii SHILOLE na DIAMOND
PLATNUMZ, tena kwa mara ya kwanza Kaka na Dada (QUEEN na DIAMOND)
watokea kwenye video moja ambayo imetengenezwa hapa hapa nchini Tanzania
na muandaaji wa video JERRY MUSHALA.
Wasanii watakao msapoti QUEEN DARLEEN siku hiyo ya
tarehe 06 April, ni pamoja na WAKAZI, BARNABA, MWASITI, AMINI, NASRY, VJ
PENNY, RECHO, CINDY RULZ, PIMP SITTA, HERO na wasanii wenginge wengi
utawaona kama Surprise, pia Bongo movies artists kama WOLPER, RADO na
wengine kibao kwenye RED CARPET.
Kiingilio kitakuwa TZS. 10,000/- tu mlangoni pale Bilicans siku hiyo ya tarehe 06. Hii si shoo ya kukosa.
Post a Comment