MWIGIZAJI mwenye mvuto Bongo, Yobnesh Yusuph
‘Batuli’ amewataka wasanii wenzake wabadilike na kuvaa kama yeye kwani
muda wa kuvaa nusu utupu umepitwa na wakati.
Mwigizaji mwenye mvuto Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’
Akizungumza na paparazi wetu baada ya kutupia picha yake aliyovaa
gauni refu mtandaoni, Batuli alisema: “Muda wa kuvaa utupu umepita,
wasanii tunapaswa tubadilike kwani kila siku tumekuwa tukisemwa vibaya
na jamii.”
Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ akiwa kwenye pozi.
Batuli aliongeza kuwa, kama kila msanii wa kike atavaa kiheshima, wataheshimiwa na kuwa mfano wa kuigwa.
Post a Comment