Selena Gomez ameamua kumrudia Mungu kwa kuanza kwenda kanisani
mara kwa mara ili kuepuka kurejea tena rehab kwa matatizo ya msongo
mkubwa wa mawazo.
![Selena-Gomez-Photoshoot-Pictures-Wallpaper-Selena-Gomez](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/Selena-Gomez-Photoshoot-Pictures-Wallpaper-Selena-Gomez.jpg)
Chanzo kimoja kimeuambia mtandao wa HollywoodLife.com: “Selena
anajaribu kubadilisha maisha yake kwa kwenda kanisani kuepuka kwenda
rehab. Anahisi kuwa ana gap la kiroho na kwamba ndio maana anapata
tabu.”
Muimbaji huyo wa ‘Come & Get It pia ameamua kuachana na kampani
yote anayohisi ni chanzo cha mabaya kwakuwa anataka kujikita katika
career yake zaidi. Mrembo huyo anadaiwa kumpiga chini mpenzi wake Justin
Bieber wiki iliyopita baada ya kugundua kuwa hajatulia.
Miongoni mwa marafiki alioachana nao ni wadogo zake Kim Kardashian, Kendall na Kyle ambao amewaunfollow wote kwenye Instagram.
Post a Comment