Wasiojua ubaya wa vyombo vya habari msikilizeni balozi huyu wa Ubelgiji..Nimempenda


Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya KICORA, Deo Baribwegure (kulia) akitoa
maelezo kwa Balozi wa Ubelgiji nchini Koen Adams (wa tatu kushoto) kuhusu
utendaji kazi wa Radio inayoendeshwa na taasisi hiyo wakati balozi huyo
alipotembelea taasisi hiyo akiwa kwenye ziara ya siku tatu mkoani Kigoma
kutembelea miradi inayofadhiliwa na nchi yake.

BALOZI wa Ubelgiji nchini Tanzania Koen Adams amevitaka vyombo vya habari na hasa Radio na TV kuwa chachu katika kuleta maendeleo na kubadilisha maisha ya wananchi badala ya kutumika vibaya na hatimaye kuleta maafa.
 Adam alisema hayo mkoani Kigoma alipotembelea taasisi ya KICORA ambayo pamoja na mambo mengine inajihusisha na utoaji wa elimu kwa njia ya Radio na kusema kuwa vyombo vya habari vikitumiwa vizuri ni msaada mkubwa kwa maendeleo ya jamii.
 Katika hilo alisema kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikisaidia kuhamasisha jamii katika kujiletea maendeleo yao kwa haraka ambapo amewaomba wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuona namna ambavyo wanaweza kuvitumia vyombo vyao iwezekanavyo katika kubadilisha maisha ya jamii inayowazunguka na kuleta maendeleo.
 Kinyume chake alionya kuwa kilichotokea nchini Rwanda na kusababisha mauaji ya halaiki kinaweza kutokea mahali popote nchini ambapo amesema kuwa asingeomba hilo litokee tena mahali pengine duniani kwa vyombo vya habari kutumika vibaya.
 Akizungumzia kauli hiyo ya Balozi wa Ubelgiji Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya KICORA, Deo Baribwegure alisema kuwa wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na Mamlaka ya mawasilianoi nchini (TCRA) ambao wamekuwa wakisimamia kwa karibu matangazo yanayorushwa na Radio na TV mbalimbali nchini.
Deo alisema kuwa Radio yake kwa kiasi kikubwa imejikita katika kutoa msaada kwa jamii ikiwemo suala la elimu na masuala mbalimbali ya kiuchumi na hasa kwa wakati huu wa sayansi na teknolojia ambapo Radio zimekuwa na nafasi kubwa ya kusikilizwa na jamii mbalimbali.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo alisema kuwa bado taasisi yake ambayo imekuwa ikijiendesha bila faida inakabiliwa na changamoto ya kupata mtaji wa kuifanya Taasisi hiyo kuendesha shughuli zake kikamilifu.
 Aidha ametoa shukrani za dhati kwa serikali ya Ubelgiji na wananchi wan chi hiyo ambao wamekuwa na msaada mkubwa katika kusaidia shughuli mbalimbali za taasisi hiyo ambazo zimekuwa zikipata misaada na ufadhili kutoka nchini Ubelgiji.
 Source Journalist press Kigoma

Post a Comment

Previous Post Next Post