Waziri
wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa akifungua
mkutano wa siku mbili wa wadau wa Teknolojia ya habari na mawasiliano
(TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa Bonde la ufa leo jijini Dar es
salaam.
Na Eleuteri Mangi- Maelezo
Serikali imejenga mazingira mazuri kwa wawekezaji ili kuvutia makampuni mbalimbali kuwekeza kwenye sekta ya mawasiliano nchini.
Kauli
hiyo imemtolewa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof.
Makame Mbarawa alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau
Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa
Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.
“Nawasihi
wajasiriamali katika mambo ya TEHAMA ndani ya nchi washirikiane na
wenzao wa nje ya nchi ili waweze kujijengea uwezo wa kukuza uchumi wa
nchi yetu” alisema Prof. Mbarawa.
Prof.
Mbarawa aliwasihi washiriki wa mkutano huo kuwa Tanzania inawakaribisha
wawekezaji kuja kuwekeza katika TEHAMA ili kuhakikisha Watanzania wote
wanapata huduma ya mawasiliano katika maeneo yote nchini hadi vijijini.
Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia John Mngondo
(kulia) akiwa miongoni mwa washiriki wa mkutano wa siku mbili wa wadau
Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa
Bonde la Ufa leo jijini Dar es salaam.
Aidha,
Prof. Mbarawa alizitaja changamoto zinazoikabili sekta ya TEHAMA ni
pamoja na ukosefu wa nishati ya umeme vijijini, kumudu gharama za
uendeshaji, ukosefu wa vifaa vya sekta hiyo na usalama wa taarifa
mbalimbali katika mitandao.
Kwa
upande wake Waziri wa Mawasiliano, Habari na Uhusiano wa Bunge kutoka
Burundi, Tharcisse Nkezabahizi alisema kuwa TEHAMA ni moja ya Nyanja
muhimu inayotumiwa katika nchi yake ikiwemo elimu na huduma za afya
ambapo ni muhimu kwa nchi za bonde la ufa kutumia teknolojia hiyo ili
kukuza uchumi wan chi husika.
Naye
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Digital Network Oy nchini Finland,
Cipa Ojala alisema kuwa mkutano huo umekuja wakati mwafaka ambapo nchi
nyingi zinatumia fursa iliyopo ili vyombo vya habari ikiwemo televisheni
kuhama kutoka analogia kwenda dijiti.
Tanzania
mpaka sasa imekuwa miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika
kutekeleza hatua ya kuhama kutoka mfumo wa analogia kwenda dijiti mbapo
hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu takribani mikoa yote itakuwa imezima
mitambo ya analojia kwenda dijiti.
Nchi
zinazoshiriki katika mkutano huo ni Burundi, Rwanda, Somaliland,
Zambia, Sudani Kusini ikiwemo Tanzania ambayo imekuwa mwenyeji wa
mkutano huo kwa mara ya pili mfululizo pamoja na wadau wengine katika
sekta hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirika la Digital Network Oy nchini Finland, Cipa Ojala
akisisitiza umuhimu wa mkutano wa wadau wa TEHAMA katika nchi za Bonde
la Ufa na msatakabali wa vyombo vya habari ikiwemo televisheni kuhama
kutoka analogia kwenda dijiti.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa wadau wa TEHAMA kutoka nchi za Bonde la Ufa
wakimsikiliza Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame
Mbarawa (hayupo pichani) akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau
Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa
Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.
Baadhi
ya washiriki wa mkutano wa wadau wa TEHAMA kutoka nchi za Bonde la Ufa
wakimsikiliza Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame
Mbarawa (hayupo pichani) akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau
Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa
Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (katikati)
akisalimiana na baadhi ya washiriki mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa
wadau Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za
ukanda wa Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.(Picha zote na Eleuteri
Mangi MAELEZO).
Post a Comment