Angelina Jolie asema anataka wanae waje kuwa wanasiasa

Angelina Jolie hataki wanae wawe waigizaji kama yeye na baba yao, Brad Pitt. Muigizaji huyo mrembo anataka waje kuwa wanasiasa.
UPI Pictures of the Year 2012 - Entertainment
Jolie mwenye miaka 38, ana watoto sita na mchumba wake wa siku nyingi Brad Pitt, 50, lakini alikiri kuwa anatumaini watafuata ndoto zingine tofauti na kuigiza. “Najaribu kuwavutia kwenye siasa. Wanangu wa kiume na w kike wanaweza kuwa na kazi zingine kubwa badala yake,”alisema.
Wapenzi hao husafiri na watoto wao wa kiume Maddox, 12, Pax, 10, na Knox, 5 pamoja na wa kike Zahara, 8, Shiloh, 6 na Vivienne, 5 wakati wakipromote filamu zao duniani kote lakini anadai kuwa anapenda waone pia sughuli za kibinadamu. Akiongea na gazeti la The Sun aisema: “Wanajua tunatengeneza filamu. Lakini pia kuwa baba yao hutengeneza samani na kujenga nyumba na kwamba mama anapenda kusafiri na umoja wa mataifa.”
Hata hivyo Angelina amewahi kumtumia mwanae wa kike Vivienne, kwenye filamu yake mpya ‘Maleficent’, wakidai kuwa wanae wengine walikuwa wakiogopa nguo zake.
Maleficent-(2014)-59 Angelina Jolie kwenye filamu ya Maleficent

Post a Comment

Previous Post Next Post