Wiki
hii haikuwa poa kwa mastaa wa Bongo ambapo alianza msanii Shaa kupigwa
na malaria siku ya tuzo za Killi zilizofanyika katika ukumbi wa Mlimani
City,ambapo alishindwa kupafomu.
Jumapili
hii msanii wa bongo fleva Rehema Chalamila ‘Ray C’ alipatwa na homa ya
Dengue mpaka akalazwa hospitali ya Mwananyamala na sasa anaendelea
vizuri na amesharuhusiwa hospitalini, akafuatia msanii wa Bongo Movie
Muhsin Awadh ‘Dr Cheni’ naye alipatwa na homa hiyo ya dengue.
Siku
za hivi karibuni taarifa zilienea kuwa staa wa filamu za Kibongo,Wema
Sepetu anaumwa,msanii huyo amefunguka kinachomsumbua na kusema kuwa
anasumbuliwa na ugonjwa wa malaria.
Chanzo:- cloudsfm
Post a Comment