MV BUKOBA Memorial 2014, Flavianna Matata na AY wahudhulia.

Ikiwa kama maadhinisho ya kila mwaka baada ya watanzania wengi sana kupoteza maisha yao katika janga hilo na kuacha majonzi makubwa katika familia zao. Mwanamitindo “Flavianna Matata” ambae na yeye ni kati ya watanzania ambao walikumbwa zaidi na msiba huo wa watanzania wote ambapo mwanadada huyo alimpoteza MAMA yake mzazi akiwa safarini ndani ya “MV Bukoba” ajali iliyotokea zaidi ya Miaka 18 iliyopita. Makumbusho haya yalihudhuliwa na wasanii wakiwemo AY, viongozi wa serikali, wafiwa, walionusurika na wananchi wengine wa maeneo hayo mjini Mwanza.
Mwanadada Flaviana Matata ambae amekuwa mstari wa mbele sana kuhusiana na kumbukumbu hizi kila mwaka huacha shughuli zake zote na kufika mjini Mwanza kuweza kuhani msiba wa mama yake na wengine wote waliofariki kwenye janga hilo. Akisindikizwa na Baba yake Mzazi “Mzee Matata”, Mwanadada huyu sio kuhani tu msiba, ila ni mmoja kati ya watu ambao wapo makini sana kuhakikisha janga kama hili halitokei tena sababu amekuwa mstari wa mbele kabisa kutoa misaada mbali mbali kuweza kuimalisha usalama wa abiria wasafirio kutumia vivuko vya mjini, ambapo Flaviana ameshawahi kutoa “Life Jackets” kwa ajili ya vivuko vinavyotumika kwenye njia hiyo.
20140521-200804.jpg20140521-200818.jpg
Baba Mzazi wa Flaviana Matata. 20140521-200921.jpg20140521-200949.jpg20140521-201001.jpg
Flaviana akiwa na mmoja kati ya walionusurika kwenye ajali hiyo.
20140521-201052.jpg20140521-201105.jpg
20140521-201139.jpg
20140521-201151.jpg
20140521-201208.jpg
20140521-201218.jpg
20140521-201244.jpg
PICHA Kwa Hisani ya Slide VISUALS

Post a Comment

Previous Post Next Post