Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Mahakama
ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa
jinsia moja ambayo ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada. (FS)
Kadhalika
sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu Uganda bali kote duniani ambapo
mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama
ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na
wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni
kinyume na sheria.
Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja
Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, tayari vilikuwa vimeharamishwa Uganda , lakini sheria hiyo mpya pia iliharamisha hatua zozote za kueneza mapenzi ya jinsia moja na wakati huu hata kuwajumuisha wanawake wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia moja. (BBC)
Post a Comment