ANGALIA JINSI CHID BENZ ALIVYOFIKISHWA LEO KATIKA MAHAKAMA YA KISUTU JIJINI DAR


Msanii wa Hip Hop, Rashid Makwiro 'Chid Benz' leo amepandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashitaka matatu ya kukutwa na madawa ya kulevya, vifaa vya kutayarishia, uvutaji wa madawa, usafirishaji na utumiaji wa madawa hayo ambayo alikamatwa nayo kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Oktoba 23, 2014.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi  Novemba 11 mwaka huu na msanii huyo ametupwa rumande  kwa kukosa wadhamini.  

Hata hivyo, atarudishwa kesho kukamilisha taratibu za dhamana ambapo wadhamini wawili walitakiwa kutoa Shs. Milioni moja kama bond. 




Post a Comment

Previous Post Next Post