Msanii Diamond (mwenye shati nyeupe) akiwa na Yamoto Band.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kwenye hafla hiyo.
WANAMUZIKI Diamond na Yamoto Band wanatarajiwa
kutumbuiza katika tamasha la Siku ya Msanii litakalofanyika Oktoba 25
mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.Akizungumza leo katika ukumbi wa Maelezo , Ofisa Uhusiano wa Siku ya Msanii (SYM) , Peter Mwendapole, amewataja wasanii wengine watakaokuwapo ni pamoja na mwanamitindo Asia Idarous, Miss Tanzania, Miss Universe na wasanii toka Kenya, Erick na Fred Omondi huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Makamu wa Rais, Gharib Bilal.
Post a Comment