Baada
ya kugundulika Dk. Craig Spencer (33) daktari aliyekuwa akihudumia
wagonjwa wa Ebola Guinea ana maambukizi ya ugonjwa huo baada ya kurejea
Marekani, nchi hiyo imeweka utaratibu maalum kwa madaktari wote
wanaorejea Marekani wakitokea Afrika Magharibi.
Utaratibu ambao umewekwa na nchi hiyo ni
ule unaowataka madaktari pamoja na watu wengine wanaotokea ukanda wa
Afrika Magharibi waliokuwa wakihudumia waathirika wa Ebola kuwekwa
karantini kwa siku 21 kabla ya ‘kujichanganya uraiani’ huko Marekani,
ambapo New York na New Jersey wameanza kuutekeleza utaratibu huo.
Zaidi ya watu 8 waliougua Ebola
Marekani, ambapo Nina Pham moja ya wauguzi waliopata maambukizi wakati
wakimhudumia Thomas Duncan aliyefariki kwa ugonjwa huo, amepona
maambukizi hayo na kupata nafasi ya kukutana na rais wa Marekani, Obama
ambaye walikumbatiana kitendo ambacho White House imekielezea kuwa ni
“namna ya kumsukuru Nina kwa huduma anayojitolea”
Imeripotiwa kuwa mtu wa kwanza
kuripotiwa kuwa na maambukizi ya Ebola New York, Dk. Spencer aliyepata
maambukizi hayo akiwa Guinea hali yake inaendelea kuimarika.
Post a Comment