Kufuatia
taarifa zilizozagaa mjini morogoro na kuripotiwa kwenye mitandao ya
kijamii kuwa mbunge wa jimbo la morogoro kusini, Dk Lucy Nkya na mwanaye
Jonas Nkya ambaye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM taifa kupitia
vijana, kurushiana risasi kwenye ofisi yao binafsi ya faraja trust fund,
watu hao wawili wamekanusha madai hayo na kudai yameleta athari kubwa
katika familia yao.
Awali taarifa zilizojitokeza na baadaye
kurushwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ilikuwa ni mama huyo
aliyewahi kuwa naibu waziri wa afya, na mwanaye ambaye ni mjumbe wa NEC
akiwakilisha vijana, kurushiana risasi kwa kugombea nyumba iliyotaka
kuuzwa jijini Dar es salaam, hali iliyofanya ITV kumtafuta kamanda wa
polisi mkoa wa morogoro Leonard Paulo ambaye kwa njia ya simu amekiri
tukio la mlio wa risasi kujitokeza katika ofisi za faraja, lakini
mazingira yake hawezi kuzungumzia hadi arudi ofisini, kwavile alikuwa
safarini.
Hata hivyo Jonas Nkya alipopatikana
amekanusha madai hayo na kwamba kilichojitokeza ni kuanguka kwa bastola
yake iliyokuwa kiunoni, baada ya kwenda ofisi za faraja kubadilisha
gari kwaajili ya kwenda shamba, ambapo ilijifyetua risasi mbili na kutoa
mlio uliosababisha baadhi ya watu kusogea eneo hilo na kwamba kama
kungekuwa na ugomvi wa kifamilia, ungefanyika nyumbani kwao ambapo yupo
kwa sasa, akimsaidia mama yake kumuuguza baba yake Prof Nkya,ambaye
amepooza, madai ambayo yameungwa mkono na mama yake mzazi ambaye naye
amehojiwa katika ofisi za faraja, baada ya kukutwa akiendelea na
majukumu yake
Post a Comment