SHAURI
la Muingreza mmoja dhidi ya mtandao wa Google , anayetaka mtandao huo kuzuia na
kuondoa taarifa zake zilizoingizwa na watu wasiojulikana zenye kumuudhi na
kumletea picha mbaya katika jamii inaanza katika mahakama kuu ya London,
Uingereza.
Muingereza
huyoDaniel Hegglin amesema katika taarifa hizo amekuwa akituhumiwa yeye kama
muuaji,anayewadhalilisha watoto na shabiki wa kundi la wabaguzi la Ku Klux Klan.
Muingerza
huyo anaitaka Google kuzuia posting hizo
kuonekana au kuingia katika hifadhi ya Google.
Aidha
katika shauri hilo Google nao wamemtaka atoe orodha ya linki anazotaka
ziondolewe, ingawa Mahakama Kuu inatarajiwa kusema kama injini hiyo katika
mtandao wa kompyuta inatakiwa kufanya zaidi.
Hegglin,
ambaye kwa sasa anaishi nchini Hong Kong, awali alikuwa anaishi na kufanyakazi
mjini London, Uingereza na alitambua kuwapo kwa taarifa hizo mbaya dhidi yake katika
mtandao mwaka 2011.
Amedai Muingereza
huyo kwamba kuna zaidi ya webu 3,600 zenye taarifa zake ambazo si za kweli na
zenye kuudhi na amesema kwamba kuorodhesha
zote kwa ajili ya Google kuzifanyia kazi zitakuwa ni gharama kubwa,
kupoteza wakati na haitasaidia.
Amesema
ingawa Google sio wenye asili na taarifa hizo, injini zake zimewezesha kusambaa
kwa taarifa hizo, na hivyo anataka mahakama kuilazimisha Google kuchukua hatua
kuzuia tarifa hizo kupatikana England na
Wales.
Mchambuzi wa masuala
ya sheria wa Shirika la Utangazaji la Uingereza(BBC), Clive Coleman amesema shauri hilo si shauri la kusahaulika
kwa kuwa linagusa usambazaji na uchapishaji wa taarifa zenye kuudhi na ambazo
si za kweli katika mtandao wa kompyuta.
Aidha
amesema shauri hilo limelenga kuangalia
ukweli kwamba mtu yoyote anaweza kuposti kitu chochoite cha kuudhi au
kumharibia jina mtu mwingine katika mtandao huku akizuia anuani yake kuonekana.
Shauri
hilo litakalosikilizwa katika mahakama kuu ya London limeelezwa kuwa shauri la
msingi litakalokuwa na athari kubwa
katika mwenendo wa injini za habari na wananchi wanaotumia.
Aidha
shauri hilo linafanyika wakati mahakama ya Jumuiya ya Ulaya nimetoa hukumu ya
haki ya kutokumbukwa, inayotoa agizo la kufutwa kwa kumbukumbu ya zamani inayoombewa kufanywa hiyo.
Post a Comment