MASELA OKOENI JAHAZI HAUSI YA JIRANI INAUNGUA!

Oyo! Inakuwa nini masela wangu wa nguvu hapo kwa fasi ya kitaa cha bee? Saidi hii mambo ni mpeto wa kutakata kama kawiz. Wanangu wa kitaa cha Bukoba poleni kinoma kwa kumlosti mzazi jembe mwanangu mwenyewe Stive.
Dah! Msela alikuwa bonge la kichwa kilichomaindi maendeleo so tumuenzi kwa kuanzia pale alipoishia. Tupo pamoko kwa sana machalii. Ebana hivi hayo maishu ya eskro si ni kurudishana bihaindi makachaa? Bati kusema ukweli kabisa yale mangawira ni parefu kinoma. Napiga stori na wana wananiteli kuwa tukizitandika dauni zile bilioni jiti tatu na ushee zinaweza kutoka Dar mpaka Roki Siti arifu. Siyo sekreti wana ni mshiko mrefu halafu eti zimelambwa na mafisadi wachache aisee.
Huko si ni kuchokoza maraia na masela tunaohaso deili mpaka naiti mazee? Yaani nimemaindi ileile.
Unanyaka hawa mafisadi wanatuchukulia poa sana bati wangejua kuwa ipo wani dei watajuta. Usicheze na jasho la maraia kozi ni laana chaliiangu.

Samu taimu nawu deizi simaindi kumingo na mastori f’lani hivi ya kuumiza moyo bati yale yanayotupunguzia mastresi. Si ndo mpango makachaa? Kaa humu sasa upate mavituzi ya kijanja.
Ebana tudei ngoja nikupe stori moo la kachaa wangu Andy B. Msela anachili aloni hapo kwa kitaa cha Mji Kasoro Bahari kwa fasi ya Moro. Muulize mwanangu Sheki. Ebana wikiendi hii natimba kitaa hiyo so kama vipi rekebisha mpango mzima tugagonge zetu nyama ya swala.

Kaka mkubwa B ni sinia bachela mzoefu. Si unajua zile za ushuani yaani kila hausi na mbwa mkali au geti? Jamaa kajibusti…kapandisha kamjengo nini na nini kwa mishe hizihizi za kuungaunga sema ana nidhamu kinoma na mambo f’lani ya fweza.
Kimbembe ni kwamba jirani yake kuna mmaza f’lani hivi mambo safi. Huku na huku yule bimdashi akaanza mambo yake. Ooh…Mara ampelekee mwana menyu kwa geto.
Mwanzoni mnyama wangu B aliogopa maana anamjua hazibendi wa maza jinsi alivyo bandindu na mara zote anakuwa na mguu wa kuku kiunoni.

Wakati jamaa yangu anataka kuchomoa, bimdashi akawa anamtoa hofu…oooh unapata problemu mambo ya kurekebisha voko jikoni mara kufua au kupiga kitu cha usafi, kama vipi niwe napika au nikuwekee kichwa cha kukupigia mausafi kozi siyo ishu za mameni. Hivi ni truu mameni hawatakiwi kudili na hizo mbishe?
Deizi za mwanzo kaka mkubwa alikuwa anachukua madikodiko anayaweka kwenye mafriji dheni yakiharibika anamwaga kozi alifili mei bii kawekewa kitu cha kumdhuru na kwamba alikuwa anamtega ili ampoteze kwenye feisi ya dunia. Si unajua tena nawu deizi ni ngumu kinoma kumtrasti mtu kisimposimpo?
Sasa kuna hiyo dei mazee jamaa anakuteli kuwa ilikuwa ni fulu drama mwanzo mwisho. Ohooo…dhati dei bimkubwa alipoibuka na msosi akamteli kachaa kuwa haondoki hadi wapige wote msosi na kushushia na kitu cha waini. Laifu linataka nini tena wakuu?
Unajua nini kilihapeni dhati dei? Kaa hapo upate ubuyu wewe watoto wa tauni noma sana.
Bimdanga akazama kwa geto freshi nini akamseti mwana kuwa asiogope kozi hazibendi wake kasafiri na makidi wapo kwenye hizi skonga za maakademi.

Wazazi msela wangu alipohakikishiwa usalama wake dheni akamruhusu jimama mkare akazama ndani. Huwezi kuamini yule mwanadashosti alikuwa na khanga moko tu na ndani hakukuwa na dokumenti ya kusapoti so kila kitu kilikwa openi kabisa wazazi.
Jamaa anakubonyezea kuwa mara bimkubwa akosee kukaa na vile ana hoja na umbo tata…wee acha kabisa. Inaitwa weka mbali na makidi wadogo. Wanangu sarakasi anazomfanyia mshikaji wangu mpaka sasa anakwambia ni sekreti yake bati masela ni bora wakatimba kuokoa jahazi kozi hausi ya jirani inaungua. Au kama vipi apigwe tu masela? Kama mbwai…mbwai tu daadeki!
Problemu mshikaji wake akimkamata mwanangu si atamtoa ubongo? Kama vipi amfungie vioo aepukane na msala usiokuwa wa lazima. Ama nini? Mmenisoma makiksi wangu? Kama vipi sii yuu neksti wiki. Nduki!

Post a Comment

Previous Post Next Post