Vurugu hizo ambazo mpaka sasa vyombo vya dola
vimeshindwa kuweka bayana wahusika wake, zilitokea mwanzoni mwa Novemba
katika mdahalo wa kujadili Katiba iliyopendekezwa uliofanyika katika
ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Blue Pearl iliyopo Ubungo mkoani Dar es
Salaam.
Vyombo vya habari viliripoti kuwa vurugu hizo
zilidumu kwa muda wa zaidi ya dakika 40 na zilitokea baada ya Jaji
Warioba aliyewahi pia kuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya awamu ya pili,
kukemea matumizi ya jina la Mwalimu Nyerere kuhalalisha Katiba
inayopendekezwa.
Bado hakuna taarifa rasmi kutoka vyombo vya
usalama kuhusu nani hasa aliratibu vurugu hizo, licha ya kuwapo kwa
hisia za kuhusika kwa kiongozi wa chama kimoja cha siasa.
Ni kwa hoja hii ya nafasi ya uwaziri mkuu kama
mojawapo ya nafasi nyeti katika uongozi wa dola, wananchi wengi
wamejitokeza wakipaza sauti zao wakilaani tukio hilo, pia kuhoji usalama
wa viongozi wastaafu.
Siyo tukio la kwanza
Hofu ya wananchi wengi kuhusu kadhia hii ya Jaji
Warioba kama mmoja wa viongozi mwenye heshima ya kipekee nchini, imekuja
ikizingatiwa kuwa kumekuwapo na matukio kadhaa hatari kuhusu usalama
kwa viongozi wakubwa nchini.
Mwaka 1972, Tanzania ilishuhudia tukio la kwanza
la kushambuliwa kwa kiongozi wa juu serikalini. Huyu alikuwa Rais wa
iliyokuwa Serikali ya kwanza ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Abeid
Amani Karume aliyeshambuliwa kwa risasi na kusababisha kifo chake katika
makao makuu ya Chama cha Mapinduzi, Kisiwandui Unguja.
Rais Karume aliuawa ikiwa ni miaka chini ya 10
tangu aongoze mapinduzi yaliyoung’oa utawala wa kisultani mwaka 1964.
Aliiongoza Zanzibar na kuipa mafanikio ya kiuchumi na kijamii kabla ya
shambulio hilo ambalo chanzo chake kiliibua hisia nyingi.
Tukio jingine katika kumbukumbu ni la mwaka 2005
linalomhusu Rais Jakaya Kikwete, kipindi hicho akiwa mgombea wa urais
kupitia CCM.
Akiwa katika moja ya mikutano yake jijini Mwanza,
alivamiwa na mwananchi jukwaani. Picha za vyombo vya habari vilionyesha
mtu huyo alikwenda jukwaani na kumvuta Rais Kikwete kabla ya wasaidizi
wake kumtoa msobemsobe eneo hilo.
Baadaye Machi 10 mwaka 2009, Rais Mstaafu wa Awamu
ya Pili, Ali Hassan Mwinyi alipigwa kibao na kijana aliyejulikana kwa
jina la Ibrahim Said katika hafla ya Baraza la Maulidi iliyofanyika
kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
Post a Comment