RAIS wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete amevitaka Vilabu vya mpira wa miguu nchini
kuwekeza katika timu za vijana wadogo walio chini ya umri wa miaka 18 ili viweze kuwa
na mafanikio ndani na nje ya nchi.
Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akizindua ujenzi wa kituo cha
michezo cha vijana wadogo walio chini ya miaka 18 kinachojengwa nchini eneo la
Kidongo Chekundu manispaa ya Ilala.
“Katika nchi yetu, timu
ya soka ya taifa haifanyi vizuri na michezo mingine nayo
vivyo hivyo, vilabu
mbalimbali vya michezo navyo havifanyi vizuri katika michezo yao
ya ndani na nje” alisema Kikwete.
Kikwete aliendelea kusema
“Kiini cha timu yetu ya soka ya taifa na vilabu vyetu
kutokufanya vizuri katika
mashindano, haviwekezi katika vijana wadogo”.
Katika kufanikisha adhima
ya kuwa vilabu na timu ya taifa ya mpira wa miguu kuwa na mafanikio, Rais
Kikwete amewaagiza viongozi Shirikisho la Mpira wa Miguu na wa vilabu vya mpira
wa miguu nchini watekeleze majukumu yao ipasavyo ili soka la Tanzania liwe la
mafanikio kwa wachezaji mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
Aidha, amelishauri
Shirikisho la mpira wa miguu nchini kuweka utaratibu ambao
utailazimu kila timu kuwa
na timu ya vijana wadogo kama ilivyo katika mataifa mengine duniani ambapo kwa
mataifa hayo, suala la kuwa na timu ya vijana wadogo na uwanja wao sio la
hiyari.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Mtendaji wa Timu ya soka ya Sunderland ya nchini Uingereza ambao ndiyo
watakaotoa wataalamu wa michezo watakaofundisha katika kituo hicho Bi. Margaret
Byrne amesema kuwa kituo hicho kitakuwa na uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa
wenye ukubwa wa mita 100×60,viwanja viwili vya mpira wa kikapu, sehemu ya kuegesha
magari 20 na kituo cha daladala, kiwanja cha kuchezea watoto.
Bi.
Margaretalisisitiza kwa ndani ya kituo hicho, kutakuwa pia na jengo la
utawala,
vyumba vine vya wachezaji
kubadilishia nguo vikiwa na vyoo na bafu, vyumba viwili vya wafanyakazi pamoja
na chumba cha chakula ambacho kitaendana na madhari ya kituo hicho.
Naye Mkurugenzi Mtendaji
wa kampuni ya Symbion ya nchini Marekani Paul Hinks amesema kuwa kampuni yake
iko mstari wa mbele nawataendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala
mbalimbali ya kijamii ikiwemo kukuza sekta ya michezo nchini kwa kujenga kituo
cha soka kwa vijana wadogo.
Ujenzi huo ambao
ulizunduliwa kwa kupanda mti wa mnazi unatarajiwa kukamilika mapema mwakani
2015 .
Source:Maelezo
Post a Comment