TCAA: Unganisheni kampuni za ndege

Kaimu Mkurugenzi wa TCAA, Charles ChachaMAMLAKA ya usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imewashauri wawekezaji wa kampuni za ndege hapa nchini kujiunga na kuanzisha kampuni moja ili kujitanua katika soko la anga.
Ushauri huo ulitolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Charles Chacha, alipokutana na wawekezaji wa sekta hiyo wanaotoa huduma katika idara mbalimbali ikiwemo chakula, usafirishaji mizigo na usafiri wenyewe.
Chacha, alisema hiyo itawasaidia kuingia kwenye ushindani wa soko na makampuni mengine ya nje kwa kuwa na ndege zenye kutoa huduma za viwango vya kimataifa.
“Utakuta kampuni ina ndege moja na pale inapopata hitilafu safari zinaahirishwa na hivyo kuleta usumbufu kwa abiria, lakini watakapojiunga zaidi ya kampuni moja adha kama hizi zitaondoka na pia itasidia kupanua mitaji yao,” alisema Mkurugenzi huyo.
Akizungumzia kuhusu mkutano huo, alisema ni utaratibu ambao wamejiwekea wakukutana na wawekezaji hao kila baada ya miezi mitatu, lengo likiwa kupitia mabadiliko mbalimbali ya sheria, kuangalia   changamoto zinazowakabili na kubadilishna uzoefu wa kazi ambazo wamekuwa wakizifanya kila siku.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Ndege, Laurence Paul, alisema bado Tanzania haijatilia mkazo wa kutosha katika usafiri wa anga ikiwemo kuunganishwa na sekta ya utalii.
Paul, alisema wakati sekta ya utalii inaongoza kwa kuliingizia fedha taifa, suala la kuinganisha na usafiri wa anga haliepukiki kwa kuwa watalii wengi wanatumia usafiri huo.
- Tanzania Daima

Post a Comment

Previous Post Next Post