
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili
jana, walidai kuwa maelekezo waliyopewa na viongozi wao wa juu ya
kuwatetea watuhumiwa ndiyo yaliyopelekea hali ya sintofahamu. Mkazi wa
Tegeta, Jerome Tesha, alisema licha ya baadhi ya wabunge wa CCM
kuonyesha msimamo wa kupinga hatua ya kuwabeba watuhumiwa lakini spika
hakuliona hilo na kushikilia msimamo wake kwani aliamini kufanya hivyo
ni kuingilia mhimili mwingine.
“Jana nilifuatilia kwa makini sakata hili, lakini
hukumu yangu moja kwa moja naipeleka kwa Spika ambaye bila kupindisha
maneno ndiye alikuwa kinara wa kuwabeba watuhumiwa hawa,” alisema Tesha.
Magreth Jonathan wa Gongo la Mboto jijini Dar es
Salaam, alisema kutokana na ukiritimba uliokithiri miongoni mwa
viongozi, wanashindwa kuchukuliana hatua wanapofanya makosa.
“ Huku kulindana kupita kiasi sijaona mantiki
yoyote kwa Spika Makinda kuwabeba watu hawa ambao kwa mujibu wa nyaraka
zilizowasilishwa bungeni zinaonyesha wazi wanahusika moja kwa moja na
ufisadi huu,” alisema Jonathan.
Sweetbert Rwabukambara wa Mbezi wilayani Kinondoni
alisema tabia ya wabunge wa CCM kulindana wameweza kumuambukiza hadi
Spika wao ambaye juzi alionyesha dhahiri kulikingia kifua suala la
watuhumiwa kuwajibishwa.
Akizungumzia suala la kukatika kwa umeme sehemu
mbalimbali nchini wakati Bunge linaendelea, alisema alitarajia jambo
hilo kutokea siku hiyo licha ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo kuagiza umeme usikatwe.
“Wakati Muhongo anawasilisha taarifa yake
hawakukata umeme, lakini juzi wakati PAC wanafanya majumuisho umeme
ulikatika, ” alisema Rwabukambara.
“Nilimsikia kwa makini sana spika ila lilipokuja
suala la kuwawajibisha watu waliohusika alisema tunaingilia mhimili
mwingine bila kutambua kuwa vitu hivi vipo wazi hata asiyesoma
anaelewa,” alisema Joseph.
- Mwananchi
- Mwananchi
Post a Comment