
Ndiyo maana nimeanza hivyo kwa kumnukuu Nyerere ambaye alikuwa akiona mbali sana katika kauli zake.
Juzi nilimsikia kocha mkuu wa Yanga, Marcio Maximo
akiwaambia mashabiki wa timu hiyo kuwa waondoe hofu kwani kiungo
mkabaji mpya aliyekuja naye kutoka Brazil, Emerson De Oliveira Neves
Rouqe ni kifaa na ana uwezo wa kucheza popote.
Maximo aliwasili Dar es Salaam katikati ya wiki iliyopita akiambatana na Emerson na kupokelewa na mashabiki wa Yanga.
Mara baada ya kuwasili, Maximo alisema hana hofu
na mchezaji aliyekuja naye kwani ni aina ya wachezaji wanaobadilika
ndani ya uwanja kulingana na aina ya mchezo. Kauli kama hiyo ya Maximo
aliitoa Julai 15, 2014 baada ya kuwasili kwa Geilson Santos Santana
‘Jaja’ wakati huo akitokea Sao Paul.
Jaja ambaye alikuwa akichezea timu ya Itabaina FC
nchini Brazil, alikuwa mchezaji wa pili kuungana na kikosi cha Yanga
baada ya Andrey Coutinho kuwasili.
Maximo alipamba kauli zake kama ilivyokuwa kwa
Jaja na juzi wakati Emerson anaingia alisema: “Mashabiki wa Yanga
hawatajutia ujio wa Emerson kwani ni mchezaji wa kimataifa, amecheza
soka nchi nyingi, ndani ya uwanjani anajua nini anafanya, ana uwezo wa
kubadilika kulingana na mchezo.”
Nakumbuka Maximo aliyempamba Jaja kabla ya
kukubali aondoke baada ya kuchemsha, juzi alirejea kumpamba, Emerson
kuwa ana uwezo wa kubadilika na kuendana na mpira.
Katika kujitetea suala la Jaja, Maximo alisema kwa
kifupi “Jaja aliondoka kwenda Brazil na huko amepata matatizo ya
kifamilia, lakini hajapata bado barua rasmi kama ameachwa, siwezi
kulizungumzia sana hilo kwani bado anasubiri barua rasmi kutoka kwa
viongozi.” Hapa ni ‘fiksi’ tu ni kwamba katemwa.
Nilifikiria mengi baada ya Jaja kuondoka,
nilifikiria mengi baada ya Emerson kuja nikiwaza tunakosea kuingia
mikataba mbalimbali, jamani hata kwa wachezaji tunabugi?
Hivi Kamati ya Ufundi ya Yanga, inamfahamu vizuri
huyu Emerson? Wakati Jaja analetwa hadi kuvuma na leo anaonekana si
lolote, ni kwamba hakukuwa na mtu anayemfahamu. Hata wewe unayesoma
hapa, ukipata dili la kufundisha popote hasa nje, ni wazi utaondoka na
mtu wako tu na ndivyo alivyofanya Maximo. Nani kati yenu Yanga anamjua
vizuri Emerson?
Ni wazi na ninaamini hivyo, Emerson atavuna dola
zake na kuondoka. Tunakosea mikataba mbalimbali ya madini, uwindaji,
uvunaji magogo na hata kwa wachezaji? Hao wamekuja kuitia klabu hasara
tu wakati kuna wachezaji wazuri Tanzania ambao hawajapewa nafasi.
- Mwananchi
- Mwananchi
Post a Comment