
Sabby Angel akiwa na Bob Junior.
STAA wa filamu za Kibongo, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ ameamua kuhama jiji la Dar kwa nia ya kumkimbia Bob Juniour ambaye hakuthamini penzi lake.

Staa wa filamu za Kibongo, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ akipozi.
Akizungumza na waandishi wetu, Sabby alisema kuwa ameona Bob Junior hamthamini ndiyo maana ameamua kukimbia na kuelekea nchini Kenya akaendelee na maisha yake kwani anao uwezo wa kukaa ‘single’ na kufanya maendeleo.
“Nimeamua kuhamia jijini Nairobi nchini Kenya ili kufanya mambo yangu ya maana, siwezi kukaa na mwanaume ambaye hana future’, Nairobi nimefungua kampuni yangu kubwa acha nifanye kazi kwanza,” alisema Sabby.
Post a Comment