Kigogo adaiwa kuzuia mshahara wake, kuongeza mkataba
* Uongozi wafunguka
* Uongozi wafunguka
Mwandishi Wetu
MMOJA wa viongozi wa juu wa Klabu ya Simba anadaiwa kuzuia mshahara wa mlinzi wa timu hiyo, Mganda Joseph Owino wakati wachezaji wenzake wote wakiwa wamelipwa.
MMOJA wa viongozi wa juu wa Klabu ya Simba anadaiwa kuzuia mshahara wa mlinzi wa timu hiyo, Mganda Joseph Owino wakati wachezaji wenzake wote wakiwa wamelipwa.
Habari za uhakika ilizonazo Jambo Leo, hadi juzi mchezaji huyo
alikuwa hajapata mshahara wake mwezi uliopita, ambapo ameambiwa atapewa
Alhamisi ijayo ikiwa haijulikani ni kwa sababu gani.
Chanzo cha uhakika kililiambia gazeti hili kuwa Owino ambaye ni
majeruhi, anaonekana kama hana mchango wowote katika klabu hiyo kutokana
na kuwa kwake nje ya kambi huku kiongozi huyo akidaiwa kumpa maneno
makali ya kumtisha.
Moja ya vitisho vinavyodaiwa kutoka kwa kiongozi huyo aliyechaguliwa
katika mkutano mkuu uliopita ni kutochezea tena Simba, yeye akiwa kama
kiongozi ndani ya klabu hiyo.
Mtoa habari huyo alisema hivi karibuni viongozi wengine walianza
mazungumzo na mchezaji huyo ambaye ni nahodha wa timu hiyo kwa ajili ya
kusaini mkataba mwingine, lakini ameonekana kutokuwa tayari kutokana na
chuki alizokuwa nazo kiongozi huyo.
Alisema hivi karibuni Owino alikutana na viongozi wakuu wa klabu hiyo
akiwemo Mwenyekiti wa Kamati ya usajili, Zakaria Hans Pope, ambao
walizungumzia mkataba mpya wa kuitumikia klabu hiyo, lakini imekuwa
ngumu kwa sababu ya kuwepo bifu (kutoelewana) kati yake na kiongozi huyo
ambaye hamtaki huku ikielezwa kuwa kiongozi mwingine katika benchi la
ufundi la timu hiyo anaonekana kuunga mkono .
Alisema hata kutoonekana uwanjani kwa nyota huyo kumechangiwa na
kiongozi huyo, ambaye aliwahi kumshinikiza aliyekuwa kocha wa timu hiyo
kabla ya kuondolewa, Patrick Phiri asimpange kwenye kikosi cha kwanza.
“Tatizo kwenye benchi kuna kiongozi anayemuunga mkono kiongozi huyo
wa kuchaguliwa kumwekea ngumu, Owino asicheze, kitu ambacho hata yeye
amekiona ndiyo maana anataka kutoka akaangalie mambo yake
mengine,”kilisema chanzo hicho.
Owino aliponea chupuchupu kuachwa kwenye usajili wa dirisha dogo
kutokana na mchezaji aliyetakiwa kuchukua nafasi yake (David Owino
‘Calabar’) kushindwa kusaini kwa wakati ikidaiwa kuwa hakuwa tayari
kujiunga na Simba.
Hata hivyo imesemekana usajili huo ulikuwa na lengo la kumkomoa
mchezaji huyo, ambaye kwa sasa anatakiwa na moja ya timu iliyopo Dubai
Falme za Kiarabu.
Kiliongeza chanzo hicho kuwa wakati wachezaji wengine wa Simba
wanapewa mshahara juzi, Owino aliambiwa atapewa wiki ijayo kwa sababu
fedha zilikuwa zimeisha.
“Ni kweli wenzake wote wamepewa lakini yeye akaambiwa mpaka wiki
ijayo, eti fedha ziliisha, tatizo kuna kiongozi hapa anatofautiana
naye, hatujui anatatizo naye gani, alisema mmoja wa wajumbe wa kamati ya
utendaji ya klabu hiyo.
Jambo Leo lilipowasiliana na Katibu Mkuu wa Simba, Steven Ali kujua
kama ni kweli kuhusu Owino kutopata mshahara, alikiri kuwa anadai wa
mwezi mmoja.
Ali alisema anachojua ni kwamba Owino alikosa mshahara kwa kuwa hakuwepo kambini , lakini mambo mengine hayajui.
“Ninachojua Owino alikosa mshahara kwa sababu ya kutokuwepo kambini
na sio vinginevyo, lakini hayo mengine mi siyajui,” alisema Owino

Post a Comment