LULU: SIJAWAHI KUWA MWEUSI



Urembo:Mrembo na mwigizaji wa filamu za kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ hivi majuzi alitupia picha yake ya zamani mtandaoni (hiyo hapo juu) ikiwa kama ni “ThrowBackThursday” (TBT) yake, na kuiandikia mameno haya;

“Let me ThrowitBack ,Shikana Mama, Enzi ZaUjana
Sijawahi kuwa mweusi lol..! Rangi Ya Mtume Nimezaliwa Nayo”
Wengi walimsifu na kumpongeza Lulu  kwa kuweza kuitunza ngozi yake kwakutupia “comments” na kugonga “likes” za kutosha kwenye picha hiyo, kwani anaonekana kuwa hatumii madawa/vipodozi ya kujichubua kama wadada wengi  wa siku hizi hutumia madawa/vipodozi ili kubadili rangi za ngozi zao.
Jiwe gizani, wewe je hautumii? Hata wa kaka nao nasikia wamo!!!!.
Mzee wa Ubuyu

Post a Comment

Previous Post Next Post