Wataalamu wa kilimo huwashauri wakulima kuchagua mbegu bora za
kupanda kwenye udongo mzuri ulio na rutuba, ili zizae na kuleta mavuno
yenye faida.
Nao wanasiasa wanautazama mwaka huu 2015 wa
Uchaguzi Mkuu kama shamba lililo na rutuba, lakini mkulima hana uhakika
na mbegu alizoshika mkononi kwamba ni ipi itampa matokeo mazuri.
Ni ukweli usiofichika kwamba kwenye miaka ya
karibuni, vyama vya siasa vimekuwa vikitumia fedha nyingi kwenye
mikutano yao na ndani na nje, ili kuhakikisha kuwa mtu anayechaguliwa na
chama anakibeba kwa kuzaa matunda mema ya kupata madaraka, jambo ambalo
linatia shaka.
Akiwasilisha matokeo ya utafiti uitwao
‘Upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ushindani wa kisiasa’, Profesa Mohabe
Nyirabu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anasema ongezeko la matumizi
makubwa ya fedha kwenye vyama vya siasa linatia shaka.
Anasema kuwa kwa jumla vyama vya siasa vipo katika
wakati mgumu ‘vikihaha’ kutafuta fedha nyingi za kufanyia kampeni na
kutafuta wanachama wapya, lakini huku vikipoteza imani yao mbele ya
wananchi kuhusu matumizi ya fedha.
Profesa Nyirabu anasema kuwa matumizi ya fedha
nyingi kwenye vyama vya siasa yameongezeka zaidi baada ya kuanzishwa
kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini.
“Kama matumizi ya fedha nyingi na utoaji wa rushwa
umekithiri katika jamii, zinatakiwa sera zinazosimamia matumizi ya
fedha ndani ya vyama hivyo ziboreshwe,” anaeleza Profesa Nyirabu.
Msomi huyo kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa na
Uongozi wa Umma ya Udsm, anasema katika nchi yenye mfumo wa
kidemokrasia, umma huvichangia fedha vyama kwa sababu kuu tatu.
Sababu ya kwanza ni kwa ajili ya kuviwezesha vyama
hivyo kukua na kusambaza itikadi na sera zake kwa wanachama wake. Pia,
michango ya fedha hukipa chama uhakika wa kuendelea kuwapo na kukinusuru
na ushawishishi kukisambaratisha. Anataja lengo la tatu la michango
hiyo kwa vyama vya siasa kuwa ni kuviwezesha kusimama kidete dhidi ya
ushawishi kutoka taasisi binafsi na mashirika ya kigeni.
Profesa huyo anasema kwamba kwa kuwa baadhi ya
vyama vya siasa vinaonekana kutumia fedha nyingi kuliko mapato
yanayopatikana, kuna haja ya vyanzo vya mapato hayo kuwekwa bayana.
“Kuwa na mapato kwenye vyama vya siasa siyo jambo
baya, matokeo ya mara kwa mara ya rushwa kwenye uchaguzi ni dalili za
kuwapo kwa tatizo linalohusu matumizi ya fedha nyingi kwenye siasa,”
anasema Profesa Nyirabu.
Matokeo ya utafiti huo yanaeleza kuwa wakati wa
mfumo wa chama kimoja cha siasa, mapato kwa ajili ya kuendesha chama
hicho yalitokana na michango kutoka kwa wanachama

Post a Comment