Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe amesema
sababu zinazofanya CCM kupoteza kura katika uchaguzi mkuu wa urais na
wabunge mwaka huu ni pamoja na kuwa na mipasuko ama makundi ndani ya
chama .
Mwakyembe aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na wanahabari pamoja na kutembelea taasisi zilizo chini ya wazira yake, ikiwamo uwanja wa ndege wa Nduliwa mjini Iringa.
Pamoja na kutembelea uwanja huo na baadae kuzungumza na wadau wa usafiri wa mkoani hapa, aliwataka viongozi wa mamlaka ya viwanja vya ndege mkoani Iringa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa kushughulikia tatizo la wavamizi wa eneo la uwanja.
Alisema kuwa uwanja wa ndege wa Iringa ni miongoni mwa viwanja 11 ambavyo vipo katika mpango wa kufanyiwa marekebisho makubwa katika awamu hii ya mpango wa ujenzi
“Serikali sasa hivi ina miradi mingi inajenga miundombinu ya viwanja vya ndege ili watu wengi waweze kunufaika na huduma ya usafiri wa anga ,tumemaliza uwanja wa Mpanda na Mafia tunajenga wa Kigoma na umefikia kwenye jengo la abiria.
“Kwa kuwa ni kiwanja cha mpakani tumeamua kurefusha uwanja kufikia kilometa tatu ili kiwe na uwezo wa kubeba abiria 150”alisema Mwakyembe na kuongeza:
“Tunaendelea na upanuzi wa uwanja wa Ndege wa Mwanza ambao utakuwa mkubwa kuliko vingine Afrika Mashariki tunajiandaa kukarabati uwanja wa Kilimanjaro na Songwe mkoani Mbeya”
Alisema Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam nao unaendelea.
Mwakyembe aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na wanahabari pamoja na kutembelea taasisi zilizo chini ya wazira yake, ikiwamo uwanja wa ndege wa Nduliwa mjini Iringa.
Pamoja na kutembelea uwanja huo na baadae kuzungumza na wadau wa usafiri wa mkoani hapa, aliwataka viongozi wa mamlaka ya viwanja vya ndege mkoani Iringa kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa kushughulikia tatizo la wavamizi wa eneo la uwanja.
Alisema kuwa uwanja wa ndege wa Iringa ni miongoni mwa viwanja 11 ambavyo vipo katika mpango wa kufanyiwa marekebisho makubwa katika awamu hii ya mpango wa ujenzi
“Serikali sasa hivi ina miradi mingi inajenga miundombinu ya viwanja vya ndege ili watu wengi waweze kunufaika na huduma ya usafiri wa anga ,tumemaliza uwanja wa Mpanda na Mafia tunajenga wa Kigoma na umefikia kwenye jengo la abiria.
“Kwa kuwa ni kiwanja cha mpakani tumeamua kurefusha uwanja kufikia kilometa tatu ili kiwe na uwezo wa kubeba abiria 150”alisema Mwakyembe na kuongeza:
“Tunaendelea na upanuzi wa uwanja wa Ndege wa Mwanza ambao utakuwa mkubwa kuliko vingine Afrika Mashariki tunajiandaa kukarabati uwanja wa Kilimanjaro na Songwe mkoani Mbeya”
Alisema Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam nao unaendelea.
CHANZO:
NIPASHE

Post a Comment