Kama umepitwa na show ya Mkasi,
 hii ilikuwa ya Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, mengi 
kayazungumza humu ikiwemo ishu ya kutangaza kugombea Urais, Escrow, 
skafu yake na pia kamtaja kingozi wa upinzani anayemvutia.
Ishu ya kutamani kugombea Urais; “Hata kama ningetamani kwa kiwango gani, kama sitatimiza majukumu haya niliyopewa hakuna mtu atakayeniamini…”
Rais 
wa awamu ya nne ameweka rekodi yake ya kutokulinda wahalifu… Ni Rais 
huyu huyu aliruhusu Waziri wake Mkuu ajiuzulu, ukiangalia kwenye rekodi 
ni Mawaziri wengi sana wameondoka. Mimi naamini anachotafuta ni hicho tu
 kutenda haki…” hapa alikuwa akizungumzia ishu ya maamuzi ya Rais kuhusu Escrow.

Kuhusiana na ishu ya Wafanyakazi wa TRA waliosababisha hasara ya Kodi, Nchemba alisema; “
 haiwezekani mtu anayetakiwa kuwajibika kwa Taifa hili akawa Waziri peke
 yake, hata aliyesoma kwa kodi ya Watanzania ana wajibu kwa Taifa… 
Kwenye siasa ya vyama vingi tunataka kufika hatua ili kila mtu aliyepewa
 wajibu aogope kuwasababishia hasara watu wengine…”
Ishu ya vijana kugombea nafasi za uongozi; “
 Mwenyekiti yeye anachokifanya anatengeneza succession plan ya kuwaandaa
 vijana ndani y Chama.. Kwenye maeneo mengi Serikali za mitaa vijana 
wameshinda, karibu kila eneo ambako alisimama mzee na kijana mzee 
alishindwa… Kilichotumika si ujana, kilichotumika ni kutaka pale 
pabadilishwe…”

Ishu ya kutangaza kugombea Urais; “Tutavuka mto tukifika mtoni..”
Likaulizwa swali kuhusu ile skafu yake anayopenda kuivaa; “ni
 kitu kama kigumu sana kuja kupata vazi moja ambalo litavaliwa na 
Wamasai, Wanyakyusa, Wazanzibar nadhani ni ngumu sana. Nilichokiona 
kinaweza kikafaa kwa wote ni skafu, hata mtu aliyevaa kanzu anaweza 
akaweka skafu. Mama na yeye anaweza akaweka skafu…”
Swali la kiongozi gani upande wa upinzani anamvutia; “… Zitto Kabwe, lakini kuchukua nchi bado hata yeye anajua …”
Unaweza kuisikiliza sauti yote ya Naibu Waziri huyo kutoka kwenye show ya Mkasi hapa.

Post a Comment