Serikali kuwaondoa waliovamia uwanja wa ndege wa Nduli mkoani Iringa.

Waziri wa uchukuzi Dokta Harrison Mwakyembe ameuagiza uongozi wa kiwanja cha ndege cha nduli mkoani Iringa pamoja na uongozi wa mkoa huo kubainisha mipaka ya kiwanja hicho cha ndege kwa lengo la kutambua nyumba zitakazoathirika na zoezi la upanuzi wa kiwanja hicho.
Dokta Mwakyembe ametoa agizo hilo mara baada ya kukagua kiwanja hicho nakusema kuwa wananchi wanaoishi katika eneo la kuzunguka kiwanja wanapaswa kushirikiana na serikali katika kumaliza changamto zinazoweza kujitokeza katika kutekeleza mradi huo.
 
Katika taarifa yake kwa waziri huyo meneja wa kiwanja cha ndege cha nduli Hanna Kibopile amesema kiwanja hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo gari la zimamoto,uchakavu wa miundombinu pamoja na uvamizi wa wananchi waliojenga ndani ya eneo la kiwanja.
 
Kufuatia agizo hilo la waziri Mwakyembe mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza ametoa wiki mbili kwa mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Iringa kufanya zoezi hilo la utambuzi wa waliovamia na kujenga ndani ya kiwanja hicho.

Post a Comment

Previous Post Next Post