Kwa kuhesabu kwa vidole vyako vya mkononi tu, hautawapata marais wengi bora wa Marekani na kumwacha kando James Knox Polk.
Huyu ni Rais wa 11 wa Marekani aliyeahidi
kuitawala kwa muhula mmoja tu wa miaka minne na kweli akafanya hivyo
kati ya 1845 hadi 1849.
Wanazuoni wanamchukulia Polk kama mmoja kati ya
marais bora kuwahi kuiongoza Marekani. Alikuwa mtaalamu wa kupanga sera
zake na kuzitekeleza kwa vitendo. Alikuwa rais imara zaidi wa Marekani
kabla ya vita mbili kuu za dunia.
Alikufa kwa kipindupindu miezi michache tu baada ya kuondoka madarakani.
Lakini kabla ya kifo chake, Polk aliwahi kutoa
kauli maarufu ambayo inabeba ukweli ambao kwa sasa unadharauliwa kihisia
katika nchi inayoitwa Tanzania.
Polk aliwahi kusema; “With me it is exceptionally
true that the Presidency is no bed of roses.” Kuna sentensi nyingi
zinazoweza kufafanua dhamira ya alichosema, lakini sentensi ya haraka
zaidi unayoweza kuitumia ni kwamba ‘Urais sio kazi rahisi’.
Taifa lenye nguvu
Ndani ya taifa lenye nguvu za kiuchumi kama
Marekani, urais unaonekana kuwa kazi ngumu. Lakini ndani ya Taifa
maskini; linaloendesha maendeleo yake kwa kutegemea zaidi hisani ya
wahisani, uraisi unaonekana kuwa kazi nyepesi sana.
Tunaendelea kusikia majina ya watu waliotamka au
wanaotajwa kutaka kugombea urais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania. Mengi kati ya majina haya ni mzaha mwingine mkubwa
unaotunyemelea baada ya mizaha mingi ambayo tunahangaika nayo katika
maisha ya kila siku.
Ndani ya ufunguo wa chama tawala, kuna ‘marais
watarajiwa’ ambao wana kashfa kubwa za kukwapua mamilioni ya fedha za
umma siku za nyuma.
Kuna walio madarakani ambao wanashutumiwa kutotimiza majukumu yao katika ubora au malengo tuliyojiwekea.
Kuna watu ambao hawana hata mizizi katika kuongoza
wizara zao au majimbo yao ya uchaguzi, lakini wameingia katika msafara
wa kenge. Tutasikia majina mengi kadri Januari itakavyoisogelea Februari
na Februari itakavyokuwa inaiendea Machi.
- Mwananchi
- Mwananchi
Post a Comment