WAISLAM WASEMA SERIKALI HAINA NIA KUUNDA MAHAKAMA YA KADHI


Baadhi ya viongozi wa jumuiaza Kiislam kutoka kushoto ni Rajabu Katimba, Imamu Juma Ramahani na Ramadhani Lwambo.
Rajabu Katimba  akizungumza na wanahabari. Waandishi wa habari mbalimbali wakifuatilia mkutano huo.
JUMUIA za Waislam nchini zimesema serikali haina nia ya kweli ya kuanzisha mahakama ya kadhi.
Hayo yalisema na katibu wa jumuia hizo, Sheikh Rajabu Katimba wakazi akizungumza na wanahabari leo katika msikiti wa Mtambani Kinondoni,  jijini Dar es Salaam ambapo alisema: “Malalamiko juu ya mahitaji ya mahakama ya kadhi yana historia ya kupindishwapindishwa na serikali ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM).”
Alitoa mfano mwaka 2005 ambapo serikali iliahidi kuanzisha mahakama hiyo lakini kwa ghilba nyingi serikali hiyo na chama chake cha CCM haikutekeleza ahadi hiyo baada ya kuingia madarakani, mbali na kwamba wakati wa mchakato wa katiba mpya ulipokuja asilimia kubwa ya maoni ya Waiislam ilisisitiza juu ya kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post