Waziri aagiza Dawasco iwaondoe mameneja wawili

Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla ameuagiza uongozi wa Bodi ya Kampuni ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (Dawasco), kuwaondoa mameneja wawili wa kampuni hiyo kutokana na wizi wa maji kufanyika kwenye maeneo yao.
Makalla amesema udhaifu unaofanywa na watendaji wa Dawasco unasababisha malalamiko mengi kwa wananchi. Alisema hayo jana wakati wa ziara yake ya kushtukiza aliyoifanya katika mamlaka hiyo huku akiagiza mameneja hao, Robert Mugabe wa Boko na Peter Chacha wa Kimara Temboni kuondolewa.
Katika maeneo aliyoyatembelea ya Magomeni Kagera, Kimara Temboni na Boko alishuhudia mitandao ya maji ya wizi ikiwa imefungwa maeneo ya wazi na vichochoroni.
“Kinachosikitisha zaidi ni kutokuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kwa wananchi maji yanapokosekana, siwezi kuikubali hali hii. Jana tumekamata wezi 12, nimeagiza wawatafute wengine wakatwe,” alisema Makalla.

Post a Comment

Previous Post Next Post