Nahodha
wa timu ya Liverpool Steven Gerrard amemshutumu mchezaji mwenzake Mario
Balotelli kwa kuonyesha utovu wa nidhamu pale alipolazimisha apige
mkwaju wa penalti badala ya Jordan Henderson aliyekuwa tayari anakwenda
kupiga adhabu hiyo dhidi ya timu ya Besiktas ya Uturuki.
Balotelli
alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao
1-0 katika mchezo wa ligi ya Uropa unaozishirikisha timu 32 uliochezwa
Alhamisi katika uwanja wa Anfield.
Hali hiyo ilijitokeza baada ya
kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel
Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard
ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya
mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Gerrard amesema kuwa Balotelli
alikuwa "kwa kiasi fulani kakosea" baada ya mchezaji huyo wa kimataifa
wa Italia kumnyang'anya mpira Henderson, ambaye alikuwa amejitayarisha
kupiga penalti hiyo.
Henderson alikuwa nahodha wa Liverpool dhidi
ya Besiktas, na Gerrard anaamini angekuwepo katika mchezo huo angepiga
penalti hiyo.
"Sheria ni sheria," amesema. "pongezi kwa Mario,
amefunga, lakini si vizuri kuona wachezaji wakibishana. Nafikiri Jordan
alilichukua suala hilo vizuri."
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers baada ya mchezo huo hakufafanua nani angepiga penalti hiyo
Post a Comment