MASWALI 10 KWA MBUNGE WANGU: Halima Mdee

1. Ester Jacob mkazi wa Kanisani
Kuna michango ya fedha ambayo inaibuka mara kwa mara hasa katika kipindi hiki tunachoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu, mfano tumechangishwa Sh 10,000 kwa ajili ya maabara, lakini juzi tena tumekuja kuchangishwa Sh 3,000 ambayo tutatakiwa kulipa kila mwezi kwa ajili ya ulinzi shirikishi hata kama una mlinzi unayemlipa, je, utatusaidiaje kudhibiti michango ya namna hiyo.
Jibu: Suala hilo linadhibitiwa kupitia vikao vya serikali za mtaa kwa kuwa ndiyo wanajadili na kupitisha hayo hivyo wananchi washiriki mikutano ya serikali za mitaa na kuhoji hayo. Mikutano hiyo huitishwa kila baada ya miezi miwili hivyo wananchi wahudhurie kwa kuwa wengi hawahudhurii.
2.  Yusuph Abdalah mkazi wa Darajani
Ni lini daraja la JKT njia panda ya Coca Cola Kawe litajengwa kwa kiwango cha zege ili kulifanya liwe imara?
Jibu: Kiujumla katika halmashauri ya Kinondoni tumekuta kuna changamoto nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na hiyo ni kutokana na makusanyo madogo ya Sh8 bilioni walizokuwa wanakusanya zamani kabla ya kuingia sisi. Katika fedha hizo walikuwa wanatenga Sh1 bilioni kwa ajili ya maendeleo na pale kuna majimbo matatu Kawe, Kinondoni na Ubungo. Hivi sasa tumefanikiwa kufikisha makusanyo ya Sh37 bilioni na kati ya hizo Sh13 bilioni ni za miradi ya maendeleo. Tumejenga barabara za lami mpya nne katika eneo la Mikocheni Tumejenga daraja kubwa la Nyerere. Changamoto ya hilo la njia panda tutalifanyia kazi katika mwaka huu wa fedha 2015/16, lakini kinachotakiwa kufanyika ni wananchi kuhakikisha mwenyekiti wa mtaa wa Mikocheni B kupeleka kwa WDC  ili ipitie na kuileta kwenye vikao vya halmashauri ambavyo mimi naingia ili tuweze kulishughulikia.
3. Godlove Jophrey mkazi wa Kawe.
Mimi ni miongoni mwa wananchi wengi wanaoishi Kawe ambao tulipanda mbegu DEC, lakini mambo yaliyojitokeza yametufanya wengi wetu tusijue hatima ya fedha zetu hadi leo, hivyo tumeyumba kiuchumi. Utatusaidia vipi kujua hatma ya fedha zetu?
Jibu: Suala la DEC tumelizungumzia na hivi sasa lipo mikononi mwa Serikali. Tumeomba Serikali irudishe fedha hizo kwa wananchi na sisi kama watumishi tuna mipaka yetu na hapo ndipo tulipofikia kwamba Serikali ndiyo inapaswa kuzirudisha hizo fedha kwa wananchi.
4. Gaudence Manyanga mkazi Mzimuni.
Kawe Mzimuni na Ukwamani hakuna sehemu ya kutupia taka hivyo kumekuwa na hali ya utupaji ovyo wa taka ambao unachafua mazingira na kuhatarisha afya za wakazi wa maeneo hayo, unatusaidiaje kupata eneo maalumu la kutupa taka?
Jibu: Eneo la kutupa taka ni miongoni mwa mambo ambayo tayari tumelifanyia kazi, tumeshakaa na watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa kutafuta eneo maalumu la kutupa taka kwa eneo la Ukwamani na Mzimuni

Post a Comment

Previous Post Next Post