MCHAKATO KATIBA MPYA: Hamad: Kwa nini Wazanzibari wanapaswa kupitisha Katiba

Wakati Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba ukifikia hatua ya Kura ya maoni inayotarajiwa kupigwa Aprili 30 mwaka huu, watu wameendelea kutoa maoni yao.
Wapo wanaoamini kwamba, mchakato huo hautapita kutokana na mambo kadhaa wanayoyaeleza na wengine wanaosema kuwa hawana shaka na kupitishwa kwa Katiba Inayopendekezwa katika kura ya maoni.
Mbunge wa Wawi (CUF), kisiwani Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed ni miongoni mwa watu wanaoamini kuwa Katiba Inayopendekezwa itapita. Anasema hana shaka Katiba hiyo itapita hata Zanzibar kutokana na maboresho mbalimbali yanayohusu kero za Muungano.
Anasema pamoja na kasoro nyingi zinazoelezwa, Katiba Inayopendekezwa haina tatizo kubwa, hasa ikizingatiwa kuwa kuna maeneo mengi yenye migororo baina ya Wazanzibari na Watanganyika, yamefanyiwa kazi.
“Lakini pamoja na yote hayo nishukuru kwa hatua iliyofikiwa. Ningeomba kwanza, vyombo vya habari vijaribu kueleza na upande wa mazuri yaliyopitishwa kwenye rasimu hiyo...Kwa mfano suala la mafuta ambalo lilishindikana kwa miaka mingi tangu enzi za Rais Hayati Karume, lakini limewezekana sasa kwa Rais Dk Shein,”  anaeleza.
Hamad anaeleza kuwa Katiba Inayopendekezwa imeingiza mambo mengi ya msingi ambayo yalikuwa kilio cha Wazanzibari, hivyo kustahili kupigiwa kura ya ndiyo, tofauti na madai ya wengi kwamba haifai.
“Katiba imeingiza mambo yote ya msingi yaliyokuwa yakipigiwa kelele na Wazanzibari. Wengine wanasema Katiba imevunjwa na Zanzibar, lakini siyo kweli ifahamike kwamba yapo mambo yanayounganisha kikatiba na mengine ni makubaliano,” anasema na kuongeza:
“Nitakupatia mfano, Cubeq waliingia kwenye kura ya maoni mara sita sasa tangu walipohitaji kujitoa Canada, lakini waliambulia asilimia 49, walipohojiwa tatizo nini? Wakasema tatizo ni uwakilishi basi wakapewa nafasi ya kuiwakilisha Canada kupitia Unesco je wamevunja Katiba?”
Anaendelea “Ni kama wanandoa, mambo mengi wanakubaliana ambayo ni kinyume na ndoa yao, je ndoa inakuwa imevunjika?”
Hamad anasema siyo kila kitu kinaweza kuingia kwenye Katiba na hata madai ya Wazanzibari yatamalizwa kwa hatua. Muungano ni damu siyo Katiba hebu angalia Watanganyika ambao ni asilimia 60 wanaoishi Zanzibar leo hii tukivunja Muungano tutawapeleka wapi?”
Kwa mujibu wa Hamad, Wazanzibari wanahitaji mikopo na misaada bila vikwazo na kama hivyo vikipatikana, kilichobaki na mambo ya utawala.
Anabainisha kwa mchakato wa mabadiliko ya Katiba ulionekana kuvurugika kutokana na mgawanyiko uliojitokeza kwenye Bunge la Katiba, lakini katika uhalisia wake, hauna matatizo mengi

Post a Comment

Previous Post Next Post