CHADEMA yazindua ‘Shahada mkononi delete CCM ’

Mwenyekiti wa chama Chadema Freeman Mbowe.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe wamezindua operesheni ya vijana wa chama hicho inayojulikana kama ‘Shahada mkononi delete CCM’.
Aidha, operesheni hiyo  itasimamiwa na baraza la vijana wa chadema ( Bavicha ), katika mkutano huo Mbowe amewataka watanzania kuacha kujengeana chuki za kisiasa na kuwa na upendo kama taifa moja kwani vyama vya siasa ni mambo ya mpito.
Akizungumzia lengo la operesheni hiyo iliyozinduliwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya mahakama ya mwanzo nguzo nane mjini Shinyanga Freeman Mbowe amesema  ni kuwahamasisha vijana wenye umri wa kupiga kura kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa oktoba mwaka huu.
Amewasisitiza  wananchi  juu ya kuchagua viongozi bora watakaowaondoa kwenye lindi la umaskini uliokithiri, kuleta haki na usawa kwa watu wote bila ubaguzi pamoja na kujenga jamii iliyo huru kiuchumi kwa kutumia fursa mbalimbali zitokanazo na raslimali za taifa.
Baada ya uzinduzi wa operesheni hiyo  mwenyekiti wa Bavicha taifa Patrobas Katambi aligawa  baiskeli 17 zilizotolewa kwa uongozi wa kata zote za jimbo la Shinyanga mjini ambazo zitarahisisha zoezi la uhamasishaji wa wananchi kwenda kwenye vituo vya kujiandikisha

Post a Comment

Previous Post Next Post