Ebola:Nchi zilizoathiriwa zisaidiwe

Rais wa Liberia, Ellen Johson Sirleaf
Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ametoa wito wa kuwepo mipango ya kusaidia nchi za Magharibi mwa Afrika zilizoathiriwa kwa Ugonjwa wa Ebola.
Wito wake umekuja baada ya Sierra Leone kupatiwa kiasi cha Dola milioni 80 za Marekani ili kumaliza tatizo la Ebola na madhara yaliyotokana na Ugonjwa huo.
Shirika la fedha duniani, IMFlimeahidi kutoa msaada wa kiasi cha dola milioni 187 kwa Sierra Leone.
Takriban dola bilioni 5 zimeahidiwa kimataifa kupambana na maradhi ya Ebola.
Ujumbe wa takriban watu 600 duniani umekutana mjini Brussels siku ya jumanne kwa ajili ya mazungumzo kuhusu Ebola na mipango ya muda mrefu kupambana na Ugonjwa huo.
Takriban Watu 10,000 wamepoteza maisha kutokana na Ebola, wengi wao nchini Guinea,Liberia na Sierra Leone

Post a Comment

Previous Post Next Post