KESI YAKE NA RUGE, JIDE AHUKUMIWA

Hatimaye ile kesi ya kudaiwa kuuchafua uongozi wa Clouds Media Group na mkurugenzi wake wa vipindi na uzalishaji, Ruge Mutahaba iliyokuwa ikimkabili staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ imetolewa hukumu ambapo mwanamuziki huyo ameamriwa kutozungumza chochote (amefungwa mdomo) juu ya walalamikaji hao.
Mkurugenzi wake wa vipindi na uzalishaji, Ruge Mutahaba.
Habari za kuaminika kutoka kwenye chanzo makini zilidai kwamba hukumu ya kesi hiyo juu ya malumbano yaliyokuwa makali kati ya pande hizo, ilikamilika hivi karibuni ambapo Jide au Lady Jaydee alipewa maelekezo hayo.
Ilidaiwa kwamba staa huyo alielezwa kuwa endapo atakwenda kinyume na hukumu hiyo atakuwa amepingana na amri ya Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar iliyokuwa ikisikiliza kesi hiyo.
Staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’.
“Kesi ilikuwa ikirindima kwa muda mrefu kwenye mahakama hiyo lakini hivi karibuni imefikikia tamati,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa gazetini.
Baada ya kunyetishiwa ‘ubuyu’ huo, mwanahabari wetu alimtafuta Ruge ili kuthibitisha habari hiyo ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli kesi moja ya kututukana kwenye mitandao ya kijamii imeshatolewa hukumu na kwa taarifa ni kweli hatakiwi kuongea chochote juu yetu ila bado kuna kesi nyingine inaendelea, nafikiri maelezo mazuri zaidi nitakukutanisha na wakili wetu ndiye atakufafanulia zaidi.”
Mei, 2013, Clouds Media Group na Ruge walimburuza Jide mahakamani kwa kile walichodai kwamba alikuwa akiwatukana kwenye mitandao ya kijamii.

Post a Comment

Previous Post Next Post