TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili (2) wapya wa Bunge
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana
Innocent Sebba.
Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua
wabunge wasiozidi 10.
Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao
Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa
mamlaka aliyonayo Kikatiba.
Wabunge
ambao wameshateuliwa ni:
-
Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa
-
Mhe. Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo
-
Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro
-
Mhe. Janet Zebedayo Mbene
-
Mhe. Saada Salum Mkuya
-
Mhe. Zakhia Hamdani Meghji
-
Mhe. Shamsi Vuai Nahodha
-
Mhe. James Fransis Mbatia
Uteuzi
huu umeanza tarehe 20 Machi, 2015.
Imetolewa na:
Premi
Kibanga,
Mwandishi
wa Habari wa Rais, Msaidizi
Ikulu-Dar-Es-Salaam
26
Machi, 2015
Post a Comment