WIKI
iliyopita tuliishia kwenye dalili za tatizo linaloitwa Pelvic
Inflammatory Diseases (PID), leo tutajikumbusha dalili hiyo na
tutaendelea na upande mwingine.
DALILI ZA PELVIC INFRAMATORY DISEASES (PID) Dalili
ya kwanza ilikua ni hali ya kupatwa na maumivu makali sana wakati wa
hedhi ambayo kitaalamu inaitwa Dysmenorrheal, tulisema kwamba maumivu
haya makali wakati wa hedhi yamegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo
ni Primary Dysmenorrheal ambayo huwapata wasichana ambao hawajapata
watoto lakini pia kuna Secondary Dysmenorrheal ambayo huwapata wanawake
ambao tayari wana watoto.
Maumivu makali wakati wa
kushiriki tendo la ndoa, hii humsababisha mwanamke kukosa raha hasa
wakati wa tendo na kumsababishia akose hamu kabisa ya kushiriki tendo la
ndoa lakini hii huweza kuwa inasababishwa sana na tatizo hili la PID na
ikasababisha mwanamke huyu kukosa raha yeye mwenyewe na hata
kusababisha migogoro katika ndoa yake na kumbe kama angelijua kwamba
kuna mimea tiba ambayo husaidia sana kuondoa tatizo hili basi
angeitumia, baadaye tutaelekezana jinsi ya kuondoa kabisa tatizo hili
kwa kutumia mmea huu wa mlonge.
TATIZO LA FIGO Pia
kuna hili suala la matatizo ya figo ambalo limekuwa ni tatizo
linalowasumbua wanawake wengi sana na hii ni kwa sababu wanawake wengi
ni rahisi sana kukumbwa na tatizo la UTI yaani Urinary Truck Infections
na hii ni kwa sababu mrija wao wa kupitishia mkojo (urethra) ni mfupi
hivyo basi maambukizi ni rahisi sana kufika kwenye kibofu cha mkojo na
kusambaa zaidi hasa kwenye mirija inayokwenda kwenye figo na pia tatizo
kufika kwenye figo kwa urahisi zaidi.
Na hii ni kwa sababu wanapoenda
haja huchutama na maumbile yao kuwa karibu sana na maeneo ya hatari na
maambukizi ya UTI huweza kumpata mwanamke huyu, na sasa tatizo hili
akishalipata na kutolitibu haraka au akawa anatibu lakini hailiishi
kabisa maana kuna wakati mwanamke utakuta anasema tatizo linajirudia
mara kwa mara kumbe tu halijaisha mwilini basi inakua ni rahisi sana
kufika kwenye figo na kuanza kusumbuliwa na tatizo la figo.
Lakini mmea huu wa mlonge unaweza kukusaidia sana msomaji wetu pia tutawaelekeza jinsi ya kuutumia hapo nyumbani.
Na kwa wale ambao wamesumbuliwa
sana na tatizo hili la UTI pia wamekuwa wakijitibia sana pasipo na
mafanikio yoyote na wengine wameshachoma hadi sindano lakini tatizo hili
bado linawasumbua basi ni vyema wawasiliane nasi kwani tuna mimea tiba
mingi kwa ajili ya kutatua tatizo hili la UTI.
Kwa ushauri vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.
Itaendelea wiki ijayo
Kwa ushauri vipimo na tiba dokta anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.
Itaendelea wiki ijayo

Post a Comment