MUME
wa mwigizaji Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuz’, Gadna Dibibi amefunguka
kuwa kamwe hawezi kukubali ndoa yake ivunjike kirahisi, atapambana hadi
dakika ya mwisho.Kauli hiyo ya Gadna ameitoa ikiwa ni siku chache tangu
vyombo vya habari viripoti kuwa wawili hao waliooana mwaka 2013,
wamemwagana na kila mtu anaishi kivyake.
“Sijampa talaka Jack hivyo bado ataendelea kuwa mke wangu halali,
nitahakikisha hilo linabaki kuwa hivyo. Kama kupishana kauli,
tulipishana na ni vitu vya kawaida lakini haiwezi kuwa ndiyo mwisho wa
uhusiano wetu labda ningekuwa nimempa talaka,” alisema
Gadna.Alipotafutwa Jack ili kusikia kauli yake kuhusu ishu hiyo,
alisema: “Sitaki kuzungumzia hilo nipe muda kidogo.”
Post a Comment