MWENDO WA KUFUNIKANA …Ronaldo aipiku rekodi ya Messi michuano ya Ulaya

Cristiano Ronaldo amefungia Real Madrid magoli mawili katika mchezo wa Ligi ya mabingwa dhidi ya Schalke 04 na kuipiku rekodi ya mpinzani wake mkubwa Lionel Messi.
Ronaldo anafikisha mabao 78 katika Ligi ya mabingwa (pamoja na UEFA Super Cup) huku Messi akiwa na magoli 76.
Lakini nyota huyo wa Ureno analingana na Messi katika kufunga magoli mengi kwenye Ligi ya Mabingwa (ukiondoa hatua ya mchujo) ambapo wote wametikisa wavu mara 76.
Ronaldo mwenye umri wa miaka 30 anaweka rekodi nyingine na kuwa mchezaji wa kwanza wa Real Madrid kufunga magoli 40 na zaidi katika msimu mmoja kwa misimu mitano mfululizo.
Messi atakuwa na nafasi ya kumpiku Ronaldo Machi 18 wakati Barcelona itakapoikaribisha Manchester City kwenye mchezo wao wa marudiaono wa Ligi ya Mabingwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post