Unaujua mpira wa ‘Chandimu’..??? usome hapa kidogo!

Na Andrew Chale wa Modewji blog
Tanzania ni miongoni mwa Taifa ambalo limekuwa likikua kila kukicha kwa kila Nyanja ikiwemo Elimu, biashara na Uchumi wake kwa ujumla ambapo mbali na vitu hivyo pia suala la michezo ikiwemo mchezo wa mpira miguu ama soka, umekuwa na mageuzi yake pia.
Tukija katika suala hilo la mageuzi katika soka, ni pamoja na matumizi yake ya nyenzo zilizokuwa zikitumika, ikiwemo mpira katika dimba. Enzi hizo mpira uliokuwa ukitumika ni wa kufuma na makaratasi ambao ni maarufu kama mpira wa Makaratasi au ‘Chandimu’.
Mpira wa Chandimu umekuwa ukichezwa kwa miaka mingi sana, ambapo kwa mujibu wa watu waliokua wakicheza miaka ya nyuma ya mwishoni mwa miaka ya 1970 hadi 80 na 90 wengi wao walikuwa wakichezea mpira huo wa Chandimu.
Pia karibu wanasoka wengi waliowika miaka ya 1990 hadi 2000, walikuwa hodari katika soka la mchangani ambalo asilimia kubwa walikuwa wakitumia mpira wa Chandimu.
Hali ya hatua hii ya kuchezea mpira wa Chandimu, inaenda sanjari na hatua ya mwanafunzi  mdogo shuleni katika darasa la kwanza hadi la tatu kuwa ambaye anatumia penseli kuandikia kazi zake, lakini endapo atakuwa ana akili nyingi na pia mwandiko wake ni mzuri, basi mwalimu humbadilishia kutoka hatua ya kuandikia penseli hadi kuandikia Peni.
1476084_10205676257135305_3562159254232846358_n
Mfano mzuri mimi ninayewachambulia hapaa:  Nilipokuwa darasa la tatu, Mwalimu alinihitaji kutumia peni kwani  mwandiko ulikuwa ni mzuri sana nilifurahia katika hatua hiyo kwa mwalimu wangu huyo wa somo la Kiswahili la kunitaka kutuimia peni, kwa tukio la kuacha kutumia penseli na kuanza kutumia peni, nililifurahia sana  kwa upande wa darasani, Lakini nilikuwa nachukia sana kwa upande wa michezo kwani nyumbani nilikuwa nacheza mpira wa makaratasi kwa timu ya watoto vijana wenzangu, wakati huo huo watoto vijana wengine waliokua hodari wa kucheza mpira wao walikuwa wakichezea mpira wa ‘gozi’ yaani mpira wa  kisasa wa kununuliwa dukani.
Suala hili liliniuma sana hivyo nilikuwa nikijitahidi kucheza mpira mzuri ili tu niweze kuchaguliwa kwenye timu ya wakubwa  na mimi nichezee ‘gozi’ niachane na Chandimu.
Kwa hali hiyo  kutoka matumizi ya Chandimu yaani mpira wa Makaratasi kwenda kutumia gozi yaani mpira wa dukani, ilikuwa na changamoto nyingi sana kwani uwezo wako ndio unaohitajika kukutoa hatua moja hadi nyingine ni sawa mfano huo  hapo wa kutumia penseli na kisha ukiwa na mwandiko mzuri na bila kufuta futa unahamishiwa kuandikia peni.
Mpira wa Chandimu
Hii ni dondoo tu kuhusiana na mpira huu wa makaratasi au Chandimu, ambao pia ilikuwa ukitoa ajira mbalimbali kwa watoto kipindi hicho kwani nakumbuka hadi mimi mwenyewe niliwahi kuwa mfumaji mzuri wa mipira hii. Nakumbuka tulikuwa tunaenda Kariakoo jioni kuokota kamba na mifuko ambapo tukirejea na mirundo ya mifuko aaaaah ukija kufuma mpira unapata mpira mmoja tu ama miwili.
Unayopaswa kujua mengine.
Mfuma mipira wa Chandimu  lazima apangwe hata kama hajui kucheza mpira.
Ukiwa unapiga ‘madochi’ sana yaani unapiga mashuti kwa kutumia dorl gumba  lazima utakuwa unatengwa kwani unatoboa/unafumua mipira.
Mipira hii asilimia kubwa ilikuwa ikichezewa barabarani, wakati huo kwenye barabara za mitaa huku kama ni uwanja basi si uwanja wote ukiwa mkubwa.
Mpira wa Chandimu ukichakaa ndio unakuwa mzuri tofauti na ulivyokua mpya.
Mcheza Mpira Kwedikabu
Unakumbuka nini
Unakumbuka nini.

Post a Comment

Previous Post Next Post