Bongo wengi waoga kupiga picha kwenye zuria jekundu katika ‘Event’

Mama wa Mitindo Tanzania na Mkurugenzi Mkuu wa Fabak fashions ya Mikocheni kwa Mwalimu Nyerer, Asia Idarous Khamsin  akipita kwa madaha kwenye zuria jekundu.
Mama wa Mitindo, Asia Idarous anaeleza kuwa, desturi ya kupita kwenye zuria inampa muhusika kujiamini hasa akiwa kwenye muonekano wa aina yoyote ile. Hali hiyo imepelekea ‘event’ nyingi zinazofanyika hapa Nchini na nchi zingine kuwa  na utaratibu maalum ikiwemo kupamba eneo la kuingilia ili wanaohudhulia tafrija ama tukio maalum kupita hao na kupata picha ya ukumbusho.
Hata hivyo Modewji blog, imekuwa ikifanya utafiti kwa muda mrefu ambapo imebaini kuwa wengi wa watanzania wamekuwa hawana desturi ya kupata ‘ukodaki’  yaani picha ya ukumbusho katika shughuli wanazohudhulia.
Licha ya kuwa wapo wanaopenda kupata picha  kwenye zuria jekundu ‘red carpet’ bado muhitikio ni mdogo hasa kwa watanzania ambao wengi wao wamekuwa na hofu ya hali ya juu bila kujua wanachoogopea pindi wanapopita kwenye zuria jekundu kiasi kwamba mtu anayepiga picha hadi amlazimishe ama amlainishe kwa maneno matamu ndio utakuta anakubali kupiga picha hiyo ya ukumbusho.
unnamed-59
Meneja wa Bang Magazine Emelda Mwamanga akipata picha na mama Wa Msanii Toka Marekani Yvonne Sangudi Kwenye Red Carpet.

Vitu ambavyo Modewji blog imevigundua

Wengi wa wanaohudhulia shughuli mbalimbali wamekuwa na ‘tabia’ ya kuongopa kuwa nimelala!,ama nipo sehemu fulani kumbe si kweli hayupo huko.
Pia inaelezwa kuwa, wapo baadhi ya wanaume ama wanawake ‘kujiachia’ na wenza ambao si wao hivyo pindi atakapopigwa picha akiwa na mwenza aliyefika naye hapo ni sawa na kujichongea.
Utafiti mwingine uliobainika ni kuwa baadhi yao kupita kwenye  zuria jekundu na kupiga picha wanajihis kama hawajapendeza hivyo kujiona kama wao si lolote. Hii imekuwa ikiwakuta watu wengi sana lakini kwa hali ya kawaida halina nguvu sana kwani Mwanadada Siyani Fadea anayefanya shughuli za  kusimamia shughuli za upambaji kwenye matamasha makubwa kwa Bara la Asia, kwenye makala yake moja alibainisha kuwa,  red carpet imekuwa ikimpa mtu ujasiri  mkubwa kwani asilimia kubwa baadhi ya mitindo,  hutokea kupitia red carpet.
“Hivyo ambavyo unavyojiona umetoka nyumbani na kujiamini, basi ujasiri huo ndio unaokupa nguvu na haki ya kuwa bora zaidi ya wengine hasa  unapopita kwenye zuria jekundu na kupiga picha kwenye wingi wa kamera na mastaa” alibainisha Siyad Fadea.
Siyadi Fadea alibainisha kuwa, ‘red carpet’ ni tukio muhimu na ambalo linatokea mara moja tu hivyomtu unapokuwa kwenye tukio na kuna red carpet basai ni muhimu wa kupata picha ya ukumbusho  na pia ni kumbukumbu ya mwandaaji wa tukio kuona ni jinsi gani alivyoungwa mkono.
DSC_0095

Dondoo zingine:

Wengi wa wandaaji wa shughuli ambazo zinakuwa na tukio la ‘Red Carpet’ wamekuwa wakijitahidi kugharamia kwa gharama kubwa  ikiwemo kukodisha ‘zuria hilo jekundu’, Pia vifaa kama taa mbalimbali kwa ajili ya kukufanya uwe ang’avu, gharama ya za kukodisha vitendea kazi ikiwemo kamera na vinginevyo sidhani kama mtu kweli unakwepa kupita kwenye red carpet.
Wapiga picha: Kwa kawaida wapiga picha wanaopiga picha za matukio asilimia kubwa wanakuwa ni wale waliopewa haki miliki na mwandaaji wa tukio, pia shughuli zingine wapiga picha maalum ambao wao kazi yao ni kupiga na kusafisha hapo hapo ambazo unazipata picha zako baada ya kuisha kwa shughuli, wapiga picha hawa pindi kama picha yako ujaikomboa/kuinunua basi picha hizo ufutwa na kutengeneza picha zingine..
Aidha, kwa sasa licha ya wengi kuogopa kupita kwenye red carpet, suala la mitandao ya kijamii hasa Instagram na facebook, imekuwa chachu ya wengi kuanza kuibuka kwa kasi kupiga picha ili kutupia kwenye kurasa zake hizo za kijamii.
AAb6Cio


DSC_0071
Rio Poul ‘The Stylish akiwa kwenye red carpet na rafiki yake ambaye naye ni mtaalamu wa kupangilia mavazi kwa models.
diamondnanelly2
Msanii Diamond Platnumz alipokuwa Marekani alipata kupita kwenye Red carpet ambayo ilikuwa ni maalum kwa watu maalufu na mastaa pekee, ambapo yeye alikuwa ni miongoni mwao hali aliyopata chansi ya kusalimiana na kupata kuhijiwa na media kubwa za nchi mbalimbali duniani.
WemaSepetuakiwaRedCapet
Wema akiwa kwenye ‘red carpet’.
AAb6xla
DSC_0106
mtvMr Flavour na kampani yake wakipita kwenye red carpet kwenye tuzo hizo.
AAb3EEl
Diamond-akiwa-katika-Redcapert
DSC_0072
s20
Asia-Idarous-na-Martin-Kadinda.
Kwa leo, niishie hapa ila nitakuja na kingine Jumapili Ijayo: Kama una picha ama habari ya tukio lolote lile, basi  tupigie 0762388056 au Whatsapp 0762388056 ama kupitia email na namba ya simu iliyopo hapo juu.

Post a Comment

Previous Post Next Post